Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya wananchi wa Kipunguni waliozuiwa kuendeleza maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, ahsante nilikuwa naomba pamoja na majibu mazuri na mambo yanayoendelea katika hii Wizara kwa hawa wananchi, nilitaka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri; ni lini hawa wananchi watapata barua ya kuwaambia kwamba sasa wanakwenda kufanyiwa tathmini upya, ni lini maana yake mlikuwa mkiongea kila siku?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nilikuwa nataka nijue ni lini hiyo tathmini itaanza kufanyika, wapate barua rasmi lakini pia wapate tarehe na mwezi ambao wataanza kufanyiwa tathmini?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bonnah Kamoli, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua ni lini barua tutapeleka kwa wananchi ili wajue, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeshakwisha andika barua kwenda Jiji na Jiji wao watachukua wajibu wa kwenda kuwajulisha na kuwahabarisha wananchi kwamba zoezi hili la tathmini linaanza rasmi, na ninaamini na kwa kuwa Jiji tumeshawaandikia tangu mwezi Aprili naamini watakuwa wamelifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, zoezi lenyewe swali lako la pili linaanza lini? Linaanza mwezi Julai na litakamilika mwezi Septemba, 2022. (Makofi)

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya wananchi wa Kipunguni waliozuiwa kuendeleza maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege?

Supplementary Question 2

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri kwamba je, fedha zilizotengwa za ujenzi wa upanuzi wa uwanja wa ndege Pemba zimejumuisha pia malipo ya fidia kwa wananchi ambao wameingia kwenye eneo hilo? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Bakar Hamad kuhusu uwanja wa Pemba; katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha utakaoanza mwezi wa Julai na tunashukuru Bunge lilipitisha tumetenga fedha kwa ajili ya upanuzi wa uwanja kwa Pemba lakini pamoja na fidia eneo lile ambalo tutatwaa kwa ajili ya ujenzi huo.

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya wananchi wa Kipunguni waliozuiwa kuendeleza maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege?

Supplementary Question 3

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona, ni kwa muda mrefu sana wananchi wa Mkoa wa Singida wameelekezwa kupisha maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha ndege Mkoa wa Singida. Nataka kujua ni lini Serikali itaanza uboreshaji na ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Mkoa wa Singida?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Kishoa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli nimemsikia mara kadhaa Mheshimiwa Mbunge akizungumzia suala la Uwanja wa Ndege wa Singida na sisi kama Serikali kupitia Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi tunasema tuainishe eneo la ujenzi wa Uwanja wa Ndege na kufanya tathmini kwa maana ya kujua gharama halisi. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 tumetenga bajeti kwa ajili ya kufanya hizo tathmini kwa ajili ya eneo la ujenzi wa uwanja wa ndege hapa Singida.