Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 350 2021-06-07

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SLYVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, ni lini Vyama vya Maendeleo ya Ushirika vya zao la mchikichi vitaanza kufanya kazi katika Mkoa wa Kigoma?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Slyvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kigoma una Vyama vya Msingi vya Ushirika wa Kilimo na Masoko 14 (AMCOS) vya zao la michikichi katika Halmashauri za Wilaya za Kigoma vipo tisa, Kigoma Manispaa viwili, Uvinza viwili na Buhingwe kimoja ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendeleza zao la michikichi.

Mheshimiwa Spika, vyama hivyo vimeshaanza kufanya kazi na kwa sasa vipo katika hatua ya kupata mkopo wa shilingi bilioni 2.9 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) utakaowezesha kuboresha mashamba ya wakulima, miundombinu ya uhifadhi mikungu ya michikichi, mashine za uchakataji na ukamuaji wa mafuta ya mawese.