Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SLYVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, ni lini Vyama vya Maendeleo ya Ushirika vya zao la mchikichi vitaanza kufanya kazi katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. SLYVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Wizara na tunashukuru kwa kupata hizo shilingi bilioni mbili tunaishukuru sana Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kutokana na uhaba wa mafuta ulioko nchini na hamasa iliyofanywa na Mheshimiwa Waziri Mkuu wananchi wa Kigoma wamehamasika sana katika kuingia kwenye zao la michikichi lakini kumekuwa na uhaba wa upatikanaji wa miche ya michikichi inafikia hatua mche mmoja unauzwa hadi shilingi 5,000.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kutoa ruzuku ya miche ya michikichi katika vyama hivi vya ushirika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Slyvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya kwamba tutoe miche bora ya michikichi kwa wakulima wa Mkoa wa Kigoma ili kuongeza uzalishaji na ninavyozungumza ni kwamba zoezi hili linaendelea katika Kambi ya JKT Bulombola, lakini vilevile pamoja na Gereza la Kitwanga ambapo jumla ya mbegu zilizozalishwa mpaka hivi sasa ni milioni tisa na miche iliyopo kwenye viriba ambayo bado kugaiwa milioni moja, lakini kwa wananchi tumeshagawa miche 970,000 ikiwa ni elekezo la Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge haya ni maelekezo ya wananchi hawa watapatiwa miche hii bure, isipokuwa tu kwa sharti la kwamba lazima wawe katika mashamba makubwa ili tuweze kui-trace miche hii na kuona inaleta tija katika nchi yetu.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. SLYVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, ni lini Vyama vya Maendeleo ya Ushirika vya zao la mchikichi vitaanza kufanya kazi katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa zao la michikichi limekuwa likifanya vizuri katika mikoa ya Kigoma, Rukwa pamoja na Katavi lakini pia hata kule Kyela inafanya vizuri sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba miche bora inagawiwa katika mikoa yote hiyo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephat Kandege, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika mikoa aliyoitaja na yenyewe ikolojia inakubali kuzalisha michikichi na mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaongeza uzalishaji wa miche ili kuweza kufikia maeneo haya yote na nichukue fursa hii pia kutoa rai kwa Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa katika mikoa ambao umeitaja kutenga maeneo makubwa ya mashamba makubwa tumeanza kuwaleta wawekezaji wakubwa kwenye mchikichi. Kwa hiyo, nitoe rai kwa wakuu wa mikoa kuhakikisha kwamba wanakuwa na maeneo ya kutosha ili wakija wawekezaji hao wawe na maeneo ya kuwapeleka na naamini kabisa kwa mkakati tulionao tutakwenda kutatua changamoto hii ya upungufu wa mafuta ya kula hapa nchini.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SLYVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, ni lini Vyama vya Maendeleo ya Ushirika vya zao la mchikichi vitaanza kufanya kazi katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona; kwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo wa wakati huo Mheshimiwa Bashe alifanya kikao Mkoa wa Kilimanjaro na akatoa maelekezo kwamba Vyama vya Ushirika vya Wilaya ya Hai badala ya kubaki na zao la kahawa peke yake viingie na mazao mengine ya mbogamboga na mazao ya biashara kama vile mgomba, vanilla na mazao mengine.

Je, ni lini Serikali itapeleka waraka maalum wa kuonyesha mfumo wa uendeshaji vyama hivi vya ushirika ili kuweza kuchukua mazao hayo yote kwa Warajis Wasaidizi na Kata zile za Boma Ng’ombe, Bondeni, Mnadani, Weruweru ziweze kunufaika na vyama hivi vya ushirika? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisa Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Waziri wa Kilimo Hussein Mohamed Bashe alitoa kauli hiyo ndani na inatekelezwa na mimi niirudie tena kwa msisitizo na kuwataka Warajis Wasaidizi wote kuhakikisha jambo hili linatekelezeka la kwamba Vyama vya Ushirika vinaruhusiwa kusimamia zao zaidi ya moja katika maeneo yao ili kuondoa multiplicity ya vyama vingi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kuhusu waraka Tume inafanyia kazi jambo hilo ili kutoa maelekezo mahsusi ambayo itawafanya Warajis Wasaidizi wote waweze kuyasimamia maelekezo hayo.