Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 351 2022-06-07

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha kuweka umeme katika vijiji 138 vilivyobaki vya Mkoa wa Simiyu?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Simiyu una jumla ya vijiji 471; kati ya vijiji hivyo, vijiji 269 tayari vina umeme na vijiji 202 bado havijafikiwa na huduma ya umeme. Vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na umeme katika Mkoa wa Simiyu vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili unaotekelezwa na wakandarasi wawili yaani M/S Sengerema Engineering Group Ltd na M/S Steg International Services. Aidha, hadi sasa jumla ya vijiji 40 kati ya 202 tayari vimeshawashiwa umeme. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.