Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha kuweka umeme katika vijiji 138 vilivyobaki vya Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; kwanza kabisa nampongeza Waziri kwa majibu mazuri sana.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 66 kwa ajili ya kujenga kituo cha kupoza umeme katika Mkoa wa Simiyu na shilingi bilioni 55 tayari zinatoka mwaka huu. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?

Swali la pili, chanzo cha maji kinachohudumia Hospitali ya Mkoa wa Simiyu kinatumia umeme wa jua siku jua halipo maji hamna hospitalini. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa TANESCO pale kwenye kituo cha afya?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka ujao wa fedha ni kweli zimetengwa shilingi bilioni 65 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Bariadi, lakini pia na line ya kutoka Ibadakuli, Shinyanga mpaka Bariadi na ujenzi huu utaanza mara moja baada ya mwaka wa fedha kuanza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kituo cha kupeleka maji katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu ambacho kinaendeshwa na solar, katika mwaka ujao wa fedha tumetenga shilingi milioni 150 ili kupeleka umeme katika kile chanzo cha maji ili kiendeshwe na umeme badala ya solar, hivyo kutoa maji ya uhakika katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu.