Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 354 2022-06-08

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepeleka shilingi milioni 260 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati 6 za Jangalo, Wairo, Humekwa, Makamaka na Ombiri. Ujenzi wa zahanati hizi umefikia hatua za umaliziaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha Zahanati za Nkulari, Nkikima, Mlongia na Handa. Aidha, ujezi wa maboma ya zahanati ya Rofat, Tumbakose na Songolo ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi bado hazijafika hatua ya lenta ili kupata fedha ya Serikali kwa ajili ya ukamilishaji.