Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Boma la Zahanati la Isusumia limemalizika tangu mwaka 2016. Naomba kujua ni lini sasa Serikali itatenga fedha ili boma lile liweze kumalizika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wilaya ya Chemba kwa ujumla ina maeneo makubwa ya kilimo na hivyo kuna wahamiaji wengi sana. Nini mkakati wa Serikali wa kujenga zahanati kwenye maeneo yale sasa wamehamia watu wengi wa kutosha? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na boma la Zahanati ya Lusubi ambayo limekamilika tangu mwaka 2016; nitoe maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Wilaya kote nchini akiwepo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, majengo yote ya kutolea huduma za afya yakikamilika ni wajibu wao kufuatilia usajili wa zahanati zile, lakini kuweka vifaa tiba vya kuanzia ilia Zahanati zianze kutoa huduma wakati tunasubiri fedha Serikali Kuu kwa ajili ya kuanza kutoa huduma kwenye vituo hivyo kwa maana ya vifaa vya ziada vinavyohitajika.

Kwa hiyo zahanati hii, itafutiwe vifaatiba mapema iwezekanavyo kupitia mapato ya ndani, lakini pia isajiliwe ili ianze kutoa huduma mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na maeneo ya Chemba ambayo yana wananchi wengi, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tunaendelea kujenga zahanati na vituo vya afya kwa maeneo ya kimkakati. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge aainishe maeneo hayo ya kimkakati Serikali ifanye tathmini na kuona mpango wa utekelezaji. Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, katika Kata ya Ihanda kuna Kijiji cha Shilanga na Seketu ambazo zina maboma ya zahanati ambayo yamekaa muda mrefu sana. Upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha maboma hayo yanakamilika ili wananchi waweze kupata huduma za afya katika maeneo hayo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze wananchi wa Jimbo la Vwawa kwa kutoa nguvu zao na kujenga maboma ya zahanati, lakini nimuhakikishie kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha mwaka mmoja zaidi ya maboma 900 ya zahanati yaliyoanza ujenzi kwa nguvu za wananchi yamekamilishwa na zoezi hili ni endelevu. Katika mwaka ujao wa fedha tuna maboma 300 ya zahanati kwa ajili ya ukamilishaji. Kwa hiyo tutahakikisha pia katika ukamilishaji huo maboma haya ya Jimbo la Vwawa pia tunayapa fedha kwa ajili ya kuanza kukamilisha kwa awamu. Ahsante.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nami nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kama ilivyo Wilayani Chemba, Jimbo la Tabora Mjini lenye Kata 29 wananchi maeneo mbalimbali katika kata hizo wamejenga kwa kujitolea zahanati ambazo sehemu nyingi wamefikia kwenye maboma. Sasa je, ni lini Serikali itasaidia hizo juhudi za wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maboma haya ya zahanati ambayo yamejengwa na wananchi katika Jimbo la Tabora Mjini ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuendelea kuyatambua kwa awamu na kuyatengea fedha kwa ajili ya kuyakamilisha. Ni sehemu ya bajeti ya maboma 300 katika mwaka ujao, tunajua hatuwezi kumaliza yote, lakini tutakwenda kwa awamu katika majimbo yote likiwepo Jimbo hili la Tabora Mjini. Ahsante.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati ya Mwaiksabe majengo yake yamekuwa ni ya muda mrefu lakini pili walikuwa hawana jengo la mama na mtoto; wananchi wale wamejenga jengo la mama na mtoto na mpaka wamepaua.

Je, Serikali ni lini itawapelekea fedha kwa ajili ya kukamilisha hatua zilizobaki kwa maana ya plasta pamoja na vifaatiba? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze wananchi hawa katika zahanati hii kwa kutoa nguvu zao na kujenga jengo la mama na mtoto na hicho ni kipaumbele cha Serikali. Naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika kukamilisha jengo hilo ili tuone kama wanaweza kutumia fedha za mapato ya ndani kukamilisha au Serikali Kuu. Lakini nikuhakikishie kwamba vifaatiba Serikali imetenga bilioni 69.9 mwaka ujao wa fedha tutapeleka pia katika jengo hilo. Ahsante.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 5

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Changamoto iliyopo katika Wilaya ya Chemba inafafana sawa na changamoto zilipo katika Jimbo la Mbinga Mjini. Kuna zahanati katika vijiji vya Mzopai, Mundeki, Mikolola, Maande na Rudisha nguvu za wananchi zimewekezwa pale. Kwa hiyo, nilitaka nijue ni lini Serikali itafanya mkakati kuhakikisha kwamba inakamilisha ujenzi wa zahanati ile?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo haya ya maboma ya zahanati katika Jimbo la Mbinga Mjini, kwanza tunawapongeza wananchi kwa kutoa nguvu zao kwa sababu huu ndiyo mpango wa maendeleo ya afya ya msingi kuchangia nguvu za wananchi katika ujenzi wa vituo hivi, lakini nimuhakikishie kama ambavyo Serikali imeendelea kukamilisha maboma katika mwaka huu zaidi ya maboma 900 ya zahanati na mwaka ujao 300; tutaendelea pia kutoa kipaumbele katika maboma haya ya Mbinga Mjini ili yaanze kukamilishwa kwa awamu. Ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa maboma ya zahanati ya Kimu, Rofat, Tumbakose, Songolo na Sori Wilayani Chemba?

Supplementary Question 6

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wananchi wa Isansa wamehamasisha kwa kutumia mapato ya ndani ya kituo cha afya wamechanga milioni 56 pamoja na matofali na mchanga; wameanza ujenzi wa wodi ya kinamama na wazazi katika kituo cha afya. Nini kauli ya Serikali katika kuwaunga mkono wananchi hawa Kata ya Insasa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kuendelea kukamilisha majengo ya zahanati na vituo vya afya, hospitali za halmashauri kwa awamu. Kwa hivyo, katika mipango hii tutaendelea pia kuhakikisha tunatambua maeneo haya ya Mbozi ili nayo yaweze kuingia kwenye bajeti kwa awamu kwa ajili ya ukamilishaji wake. Ahsante.