Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 357 2022-06-08

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto ni kituo cha daraja A kilianza kujengwa mwaka 2014 kwa gharama ya shilingi 417,000,000 na hatua iliyofikiwa ni umaliziaji. Ujenzi wa kituo hicho unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu wa Juni 2022. Nashukuru.