Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri na ni kweli kituo kile kinamalizika niishukuru Serikali kwa kutupa fedha milioni 417, lakini pia nimshukuru IGP Sirro alikuja kule na akamuomba Mkuu wa Wilaya aitishe harambee ya kuchangia majengo ya watumishi, lakini Mkuu wangu wa Wilaya alifanya hivyo na mpaka sasa hivi tunavyosema kuna zaidi ya shilingi milioni 210 kwa ajili ya kujenga nyumba za polisi namshukuru sana Mkuu wangu wa Wilaya na timu yake ya Kamati ya Ulinzi na Usalama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza; Gereza la Lushoto lipo katikati ya Mji wa Lushoto na hivyo kusababisha wafungwa wetu kukosa hata sehemu ya kuota jua, lakini wakati huo huo kuna eneo lipo nje ya mji kidogo wanaita Yogoi.

Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kwenda kujenga gereza hilo maeneo ya Yogoi na ambako ndiyo kwenye nafasi kubwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Wilaya ya Lushoto ina wakazi wengi sana kama unavyofahamu, lakini ina taasisi nyingi za binafsi na za Serikali, lakini ikitokea changamoto ya majanga ya moto huwa wanapiga simu Korogwe ambayo kutoka Lushoto kwenda Korongwe ni kilometa zaidi ya 70. Kwa hiyo, mara nyingi wananchi wetu wanapata hasara.

Sasa basi niiombe Serikali, je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu au ulazima haraka kujenga kituo cha zimamoto katika Wilaya ya Lushoto? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Shekilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru kwa kutambua juhudi za Wizara lakini na hususani Jeshi la Polisi kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa kituo cha polisi pale Lushoto. Lakini nimshukuru pia DC kwa harambee aliyoifanya kupata shilingi milioni 210 kwa ajili ya nyumba za wafanyakazi, nadhani ni jambo jema la kuigwa na maeneo mengine.

Sasa kuhusu gereza la Lushoto ambalo tunatambua liko katikati ya mji na eneo lile ni finyu ni kweli baada ya Wizara kuona changamoto hizo inayo mpango wa kuhamishia gereza hilo eneo ya Kambi ya Yogoi ambayo iko nje kidogo ya Mji wa Lushoto. Kwa hiyo, pale itakapopata fedha za ujenzi wa gereza hilo, gereza hilo tutalihamisha ili jengo lililopo lifanye kazi nyingine za kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na lingine kuhusu ombi lake la zimamoto tunalipokea ni suala tu la kibajeti tutakapo kuwa tumepata fedha tutajenga Ofisi ya Zimamoto ndani ya Wilaya ya Lushoto. Nashukuru.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; kwa kuwa Songwe ni Wilaya naomba kufahamu ni lini sasa Serikali itatujengea Kituo cha Polisi katika Kata ya Mkwajuni chenye hadhi ya Kiwilaya? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyowahi kusema kwenye majibu yetu ya msingi ujenzi wa vituo vya polisi vya wilaya na mikoa utaendelea kadri tutakavyopata fedha, kipaumbele kwa mwaka ujao ni kujenga Makao Makuu ya Mikoa na baada ya hapo tutaingia kwenye wilaya zetu. Kwa hiyo, tutakapopata fedha tutajenga ndani ya Wilaya ya Songwe. Nashukuru. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana; kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Mbeya, Jimbo la Mbeya Vijijini wameweza kujenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mbalizi na sasa kuna mahitaji makubwa ya kujenga kituo katika Kata ya Igoma na Kata ya Ilembo. Je, ni lini Serikali itaunga mkono nguvu za wananchi kwa ujenzi wa vituo hivyo viwili? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali mawili ya Mheshimiwa Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuwapongeze wananchi wa kata hizo mbili ambao wameanza ujenzi wa vituo vya polisi vya kata zao, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara itatuma wataalam kutoka Jeshi la Polisi kwa ajili ya kufanya tathimini kuona kiwango cha ujenzi kilichofikiwa, kiasi gani cha fedha kinahitajika ili kumalizia tuweze kuingiza kwenye mpango wetu wa bajeti wa kumalizia vituo ambavyo vimejengwa kwa nguvu za wananchi. Kwa hiyo, tunaomba awe na subira kidogo.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 4

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara kadhaa Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakisimama na kuomba kujengewa vituo au kukarabatiwa.

Sasa ni lini Serikali itaandaa mpango mzima utakoonyesha orodha wa vituo vinanavyotaka kujengwa au kukarabatiwa kwa nchi nzima ili kuwapunguzia waheshimiwa kusimama kuomba vituo mwaka nenda mwaka rudi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Asha Juma Mshua kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokea ushauri wako na kwa kweli Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imeandaa mpango mkakati wa kuboresha sekta ya usalama wa raia ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa majengo. Kwa hiyo, ushauri wa kuleta mwongozo hapa unaoonyesha kituo gani kitajengwa lini au kitakarabatiwa lini tutauandaa tuweze kuuleta kwa Waheshimiwa Wabunge ili kwa kweli kupunguza maswali mengi ya nyongeza ambalo jibu lake linakuwa kama vile linafanana. Nashukuru.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 5

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Halmashauri ya Kyerwa ni moja kati ya Wilaya mpya ambayo pia haina Kituo cha Polisi, hivyo OCD utumie ofisi ndogo ambayo iko Kagenyi, wananchi tayari wameanza tayari ujenzi wa kituo cha polisi cha wilaya.

Nataka nijue ni lini Serikali itawapelekea fedha ili waweze kumalizia ujenzi ambao wameuanzisha kwa nguvu zao wenyewe? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: - (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua uwepo wa halmashauri au wilaya nyingi ambazo hazina vituo vya polisi vya Wilaya kwa maana ya OCDs officce na niwashukuru halmashauri ambazo wanatoa majengo kwa ajili ya kutumiwa na wenzetu wa polisi ni muahidi tu Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo nimekuwa nikisema katika majibu ya nyongeza hapa, ya maswali ya msingi tunaendelea kujenga vituo vya polisi kwenye mikoa na wilaya ambazo hazina kabisa vituo hivyo. Kwa hiyo, Wilaya ya Kyerwa ni moja ya wilaya ya kipaumbele hasa ukizingatia kwamba iko mpakani pale ambapo itatokea tutapata fedha tutaipa kipaumbele cha juu. Nashukuru. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 6

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi; Wilaya ya Tanganyika ni wilaya ambayo ipo pembezoni mwa mipakani, ni wilaya ambayo haina kabisa kituo cha polisi na wananchi wamejiotolea kupitia hamasa ya Mkuu wa Wilaya wameanza kutoa michango ya kujenga kituo cha polisi.

Je, ni lini Serikali itawapelekea fedha ili wananchi hao waweze kupata kituo cha polisi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwishajibu kwenye suala la Kyerwa, Wilaya zote za mpakani ni kipaumbele cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuona kwamba zinapata vituo vya polisi kwa ajili ya kuimarisha usalama wa raia na mali zao. Kwa hiyo, pale ambapo tutapata fedha Wilaya ya Tanganyika itajengewa kituo cha polisi kama ambavyo tumeahidi katika bajeti yetu iliyosomwa na Waziri wangu hapa mwezi mmoja uliopita.