Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 43 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 367 2016-06-15

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-
Jimbo la Nyamagana ni jimbo pekee lililochangia mradi wa ujenzi wa nyasi bandia kupitia TFF shilingi 160,000,000.
Je, ni lini Serikali itawasisitiza TFF kuhakikisha kuwa uwanja huu unakamilika kwa wakati na kuendeleza malengo yaliyokusudiwa?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing‟oma Mabula, Mbunge wa Nyamangana kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, uboreshaji wa uwanja wa Nyamagana wa kuweka nyasi bandia ulianza mwaka 2014 ukiwa na thamani ya dola za Kimarekani 737,886 sawa na shilingi za Kitanzania 1,193,161,662. Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA) lilitoa msaada kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kiasi cha dola za Kimarekani 618,946 sawa na shilingi za Kitanzania 1,000,835,682 na Halmashauri ya Nyamangana ilichangia dola za Kimarekani 118,943 sawa na shilingi za Kitanzania 192,330,831.
Mheshimiwa Naibu Spika, nyasi hizo bandia zimegharimu tozo kiasi cha dola za Kimarekani 100,121.93, sawa na shilingi za Kitanzania 220,268,400 ikujumuisha import duty na VAT. TFF kama msimamizi wa mpira wa miguu kwa niaba ya Halmashauri ya Nyamangana na Serikali, wameshughulikia mchakato wa kutoa msamaha wa tozo hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nyasi bandi tayari zimewasili Dar es Salaam tangu tarehe 17 Aprili, 2016. Baadhi ya vifaa tayari vimeshafika katika Uwanja wa Nyamagana na mkandarasi amekwishaanza kazi ya ukarabati wa uwanja huo. TFF sasa wako katika mchakato wa kumalizia kusafirisha vifaa vilivyobaki.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na ukweli kwamba ukarabati wa uwanja wa Nyamagana kuufanya uwe wa nyasi bandia unahitaji umakini mkubwa ili uwe mzuri, imara na wenye hadhi ya Kimataifa ni lazima mkandarasi ahakikishe kuwa ubora wa viwango vinazingatiwa. Kwa vile mpango wa ukarabati huo ulitakiwa ukamilike mwishoni mwa mwezi huu, natoa wito kwa mkadarasi huyo kuhakikisha kwamba ukarabati huo unakamilika haraka iwezekanavyo ili uweze kutumika.