Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Jimbo la Nyamagana ni jimbo pekee lililochangia mradi wa ujenzi wa nyasi bandia kupitia TFF shilingi 160,000,000. Je, ni lini Serikali itawasisitiza TFF kuhakikisha kuwa uwanja huu unakamilika kwa wakati na kuendeleza malengo yaliyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri na kwa mara ya kwanza Wizara hii imeonesha uhalisia wake kwa kutoa majibu kwa vitendo nawapongeza sana.
Pamoja na majibu haya mazuri ya vitendo, Halmashauri ya Jiji la Mwanza kama ambavyo imekuwa ikishiriki kwa asilimia kubwa katika kuboresha michezo, tayari imeshaandaa ramani ya uwanja mzima na imeshaanza kupita ngazi mbalimbali. Ninataka kupata tu maoni kutoka kwenye Serikali kwamba uwanja huu pamoja na kwamba utakuwa umetengenezwa eneo la kuchezea, lakini bado tutakuwa na changamoto kubwa katika eneo la mzunguko mzima kwa ajili ya kupata vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo, lakini jukwaa kuu na maeneo ya kukaa ili uwanja ukamilike na kuwa uwanja wa kisasa. (Makofi)
Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kusaidia Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuhakikisha uwanja wa Nyamagana unakuwa ni wa kisasa na ambao unaweza kutumika na mechi za Kimataifa? (Makofi)
Swali dogo la pili tayari vifaa vimeshafika, ni lini ….
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Stanslaus naomba hilo swali la pili ufupishe kwa sababu la kwanza umelifanya refu.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini TFF waithibitishie Wizara watakuwa tayati kukamilisha uwanja huu maana tumesubiri sana na tunahitaji kuutumia haraka tunavyoweza? Nakushukuru.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ambavyo amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba uwanja huu wa Nyamagana unakarabatiwa.
Katika kufuatilia tumebaini kwamba Mheshimiwa Stanslaus Mabula alipopata nafasi ya kuwa Meya tu mwaka 2012 Septemba alihakikisha kwamba anaondoa urasimu wa utoaji wa pesa mwezi Disemba, 2012 na mwaka 2013 mchakato wa kuanza kuagiza nyasi bandia ulikamilika, kwa hiyo nampongeza sana na ninaomba Waheshimiwa Wabunge tuige mfano wa Mheshimiwa Mabula. (Makofi)
Swali lake la kwanza ambalo ametaka kujua kwamba ni vipi sasa wanaweza wakakamilisha ule mzunguko mzima wa uwanja, nimhakikishie tu kwamba Wizara yangu ipo tayari kutoa ushirikiano (technical support) ili kusudi kuweza kuona kwamba ni jinsi gani sasa vile vyumba au eneo lote linaweze likazunguka, ikizingatia kwamba ni lazima kuwepo na facilities kama za vyumba za kubadilishia nguo na vyumba vya waandishi wa habari pamoja na vyumba vya matibabu ili kusudi uwanja huu uweze kukidhi viwango vya Kimataifa. Kwa hiyo, kupitia BMT Wizara yangu itatoa ushirikiano wa karibu sana na ninaomba Halmashauri pia iwe karibu na BMT.
Swali lake la pili sasa kwamba ni lini uwanja huu utakamilika, niseme tu kwamba Serikali inafanya kazi kama timu, kwa sababu nimeshatoa wito mkandarasi afanye kazi haraka, ninaomba Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Mwanza washirikane na Halmashauri, washirikiane na TFF ili kumsimamia mkandarasi huyu aweze kukamilisha haraka ujenzi wa uwanja huu.

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Jimbo la Nyamagana ni jimbo pekee lililochangia mradi wa ujenzi wa nyasi bandia kupitia TFF shilingi 160,000,000. Je, ni lini Serikali itawasisitiza TFF kuhakikisha kuwa uwanja huu unakamilika kwa wakati na kuendeleza malengo yaliyokusudiwa?

Supplementary Question 2

MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri lakini nina swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kila mwaka Shirikisho la Mpira la Ulimwengu (FIFA) huwa linatoa goal project kwa nchi kadhaa wanachama wa Shirikisho hilo. Tanzania tumekuwa tukipata goal project za viwanja mara nyingi;
Je, Mheshimiwa Waziri atakubaliana nami sasa wakati umefika kuishawishi TFF pale walipopata goal project basi safari hii uwanja kama huu wa Mwanza wa kuweka nyasi bandia uelekee Zanzibar?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba FIFA huwa ina goal project na inatoa support ya ujenzi wa viwanja kwa kuweka nyasi bandia kupitia TFF, napenda kumtaarifu Mheshimiwa Hafidh Ali kwamba uwanja wa Gombani uliopo Pemba tayari umeshapata msaada wa kuwekewa nyasi bandia kupitia ufadhili wa FIFA. (Makofi)
Hata hivyo hii haizuii kuna vigezo pia ambavyo vinatakiwa kufuatwa ili kusudi FIFA iweze kutoa ufadhili huu. Kigezo kimoja wapo ni kwamba uwanja ni lazima uwe wa Halmashauri, pia uwe ni uwanja ambao unaweze kuchezesha mechi za Kimataifa, vilevile wahusika wa uwanja huu wawe tayari kuchangia asilimia 16. Ahsante sana.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Jimbo la Nyamagana ni jimbo pekee lililochangia mradi wa ujenzi wa nyasi bandia kupitia TFF shilingi 160,000,000. Je, ni lini Serikali itawasisitiza TFF kuhakikisha kuwa uwanja huu unakamilika kwa wakati na kuendeleza malengo yaliyokusudiwa?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri kwa mpango huu wa hizi nyasi bandia zinazotolewa, je ni mpango wa kila Mkoa na kama ni kila Mkoa, je, ni lini Mkoa wa Simiyu mtatupa uwanja wa namna hii? Ahsante sana.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na uwanja wa Simiyu vigezo ni kama nilivyovitaja kama uwanja huu ni wa Halmashauri na unakidhi vigezo vya kuwa wa Kimataifa, goal project inaweze ikasaidia, lakini utaratibu ni kwamba TFF inaandika orodha ya viwanja vitano na kuandika details zake na vinapofika FIFA wao wanateua kulingana na ushindani wa kukidhi vigezo vya kutoa msaada. Ahsante.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Jimbo la Nyamagana ni jimbo pekee lililochangia mradi wa ujenzi wa nyasi bandia kupitia TFF shilingi 160,000,000. Je, ni lini Serikali itawasisitiza TFF kuhakikisha kuwa uwanja huu unakamilika kwa wakati na kuendeleza malengo yaliyokusudiwa?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Wananchi wa Karagwe tunamkumbuka Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa push-up za kihistoria alizozipiga pale Kayanga. Je, Serikali mnaonaje kama mkitusaidia kujenga uwanja wa Wilaya pale Kayanga ili tuweze kumuenzi Rais wetu kwa ule ukakamavu alioonyesha kwa vijana wa Karagwe? Nashukuru sana

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kwamba push-up kwa mara ya kwanza zilipigwa kwenye eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge anasema, hii ilithibitisha uwezo wa Rais John Pombe Magufuli wa afya yake, lakini pia ulionyesha kwamba Serikali atakayoiunda ni Serikali ya Hapa Kazi Tu tofauti na wenzetu mgombea wao nadhani hiyo kazi ilikuwa ngumu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Wizara kwa kushirikana na Halmashauri anakotoka Mbunge tunaweze kuzungumza kuona namna ya kushauriana kuweka kumbukumbu hii muhimu ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inayofanywa. Kwa hiyo, Wizara na Halmashauri ambapo anatoka Mbunge tutakaa pamoja tuzungumze tuone namna ya kuweka hii kumbukumbu muhimu.