Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 359 2022-06-08

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro kati ya wananchi na TAWA katika Bonde la Mto Kilombero?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Jimbo la Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza kutekeleza maamuzi yaliyotolewa na Baraza la Mawaziri tangu Oktoba, 2021. Utekelezaji wa maamuzi hayo ulianza katika mikoa yenye migogoro ikiwemo Mkoa wa Morogoro hususan Pori Tengefu la Kilombero. Timu ya Wataalam ya Kitaifa ya Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi iko uwandani, inaendelea na zoezi la tathmini kwa kushirikisha mkoa, wilaya na wananchi wa maeneo hayo. Aidha, timu hiyo inafanya tathmini ya makazi na shughuli zenye athari kwenye uhifadhi wa vyanzo vya maji na rasilimali za wanyamapori ndani ya eneo la Pori Tengefu na Bonde la Mto Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utatuzi wa migogoro hiyo utaanza baada ya tathmini kukamilika.