Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 361 2022-06-08

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHWALE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza geti lingine ndani ya Jimbo la Momba kutokana na geti la Tunduma kuzidiwa katika kutoa huduma?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichwale, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kurahishisha biashara kati ya nchi ya Tanzania na Zambia na kuondoa changamoto ya msongamano wa magari katika Kituo cha Tunduma, Serikali inaendelea kuchambua na kutathmini taratibu zilizopo ili kuona kama kuna uwezekano wa kuongeza Kituo cha Forodha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuondokana na changamoto ya msongamano wa magari ambapo Januari, 2021 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) iliingia makubaliano na Mamlaka ya Mapato ya Zambia yanayoelekeza hatua mbalimbali za kuchukua kwa kila nchi. Hatua hizo ni pamoja na: -

i. Kuunganisha mfumo wa TANCIS wa TRA na mfumo wa ASCUDA World wa Zambia ili kuiwezesha Idara ya Forodha Zambia kupata taarifa za shehena ya mzigo husika kabla kuwasili mpakani; na

ii. Serikali ya Zambia kufanya maboresho ya miundombinu ya barabara na eneo la kuegesha magari kupitia ufadhili wa Trademark East Africa (TMEA).

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na makubaliano hayo, Serikali kwa upande wa Tanzania imefanya yafuatayo: -

i. Uanzishwaji wa Kituo cha Pamoja cha Forodha ambacho kimesaidia taasisi zote za Serikali kuwa sehemu moja na kuwasiliana kwa haraka; na

ii. Serikali kupitia ufadhili wa TMEA imenunua scanners tatu ambazo ni baggage scanner, body scanner na cargo scanner. Aidha, baggage scanner na body scanner zinafanya kazi na cargo scanner inatarajiwa kuanza kufanya kazi mwezi Julai, 2022, ahsante.