Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHWALE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza geti lingine ndani ya Jimbo la Momba kutokana na geti la Tunduma kuzidiwa katika kutoa huduma?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, katika majibu ya msingi ya wizara inaonesha wanazungumzia zaidi biashara kati ya nchi ya Zambia na Tanzania, lakini geti la Tunduma ninaongelea ni biashara kati ya nchi ya Zambia na nchi ambazo ziko SADC ambazo ni zaidi ya saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu ya nyongeza kama yafuatavyo; kabla ya maboresho ya bandari zetu lile ilikuwa asilimia 70 ya mizigo inapitia geti lile, kwa hiyo tafsiri yake kama tumeboresha bandari zetu na Kongo wameingia kwenye East Africa ina maana kwamba nchi zingine zitapitisha mizigo pale.

Je, Serikali haioni kuna ulazima na uharaka sana kuhakikisha wanaongeza geti lingine ili kuboresha huduma na ufanisi unaotakiwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kama ambavyo ziko nchi nyingine ambazo tunapakana nazo, mfano Kenya, kuna mageti ya forodha zaidi ya mawili au matatu, mfano Holili, Namanga, Tarakea na lile geti la Mombasa na Mheshimiwa Waziri alifanya ziara kwenye Jimbo la Momba mwaka jana.

Je, hamuoni sasa kuna haja kabisa ya kuhakikisha nchi ya Zambia ambayo inahudumia nchi zaidi ya saba ya SADC kupata geti lingine ndani ya Jimbo la Momba ili kuhakikisha tunaongeza mapato?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama yanafanana maswali yake yote mawili kwa hiyo ni suala moja na nimesema katika majibu yangu ya msingi kwamba Serikali inafanya uchambuzi na tathmini kupitia katika sehemu hiyo pamoja na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tukiona Serikali ipo haja ya kuongeza geti basi Serikali yetu ni sikivu, na iko tayari kufanya hivyo, ahsante.