Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 370 2022-06-10

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba unasafishwa, kina kinaongezwa na kingo za mto zinajengwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bernadetha Kasabago Mushashu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeshachukua hatua muhimu za kudumu za kuondoa changamoto za Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba. Kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba tayari imeibua mradi wa utunzaji wa Mto Kanoni kupitia mradi wa TACTIC unaotarajia kuanza Januari, 2023 wenye thamani ya shilingi milioni 500. Lengo la mradi ni kuondoa kero kubwa ya mafuriko ambayo hutokea kila mwaka nyakati za mvua ya masika na kuathiri zaidi ya kaya 331. Mradi huu utahusisha ujenzi wa maeneo makuu mawili ambayo ni kuongeza kina na upana wa mto; na ujenzi wa kingo za mto.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa sasa Serikali imeendelea kuchukua jitihada za muda mfupi ambapo Manispaa ya Bukoba kila mwaka hutenga kiasi cha shilingi milioni sita kwa ajili ya shughuli za kusafisha, kupanua na kuongeza kina cha mto kwa kuondoa tope, uchafu na miti.