Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba unasafishwa, kina kinaongezwa na kingo za mto zinajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mafuriko katika Mto wa Kanoni ulio katika Manispaa ya Bukoba umewatesa watu kwa miaka mingi na sasa hivi naishukuru Serikali kwa kuweza kukubaliana na ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba na sasa wanauingiza mto huu katika mradi wa TACTIC.

Je, kuna mvua za vuli zitaanza mwaka huu za mwezi Oktoba mpaka Januari; Serikali inaweza ikaongezea fedha kiasi kwenye ile milioni sita inayotengwa na Halmashauri ili kusudi angalau wakafanya ukarabati wa awali isije ikatokea tena mafuriko mwaka huu?

Swali la pili; ili kuweza kuondoa mafuriko kabisa katika mto huu, inabidi mto upanuliwe, kina kiongezwe, kuta zijengwe za mto huu kutoka kwenye Kata ya Kagondo, Rwamishenye, Amgembe, Gireye, Bakoba hadi kuingia kwenye Ziwa Victoria. Je, katika huu mradi unaokuja wa TACTIC haya maeneo yote yatazingatiwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Mushashu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mama Mushashu kwa sababu katika kumbukumbu yangu ni Mbunge mwana mazingira muda mrefu sana na hili analozungumza ni utashi kutoka katika moyo wake kabisa na nikiri wazi kwamba Manispaa imeanza kufanya kazi na Serikali kila muda tunafanyakazi, na Mama Mushashu anakumbuka kupitia mradi wa UGLSP pale katika Manispaa ya Bukoba hata mwanzo tulianza kufanya kazi hii kale kamfereji kadogo kalikokuwa kanaenda pale mpaka katika ziwa.

Kwa hiyo, tumetenga milioni sita hata hivyo tutaangalia pale itapobainika kwamba ile milioni sita ina changamoto tutaona nini cha kufanya kwa upande wa Serikali kwa ujumla wake. Lakini katika hizi kata zingine je, zitahusika vipi? Kama nilivyosema ni kwamba lengo letu ni kwamba kuondoa changamoto ya mafuriko na kama ulivyosema kweli katika kata hizi zote zinakabiliwa na mafuriko haya mto unapotokea jambo hili.

Tutaangalia katika ujenzi wa kuta katika mto huu jambo hilo lote litazingatiwa na hata kama kutatakiwa additional financing ya kuhakikisha maeneo mengine yote tuyaboreshe tutalifanya Mheshimiwa Mbunge bila shaka aina yoyote.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba unasafishwa, kina kinaongezwa na kingo za mto zinajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi; je, Serikali ina mpango gani wa kuokoa Ziwa Babati kwa kuondoa magugu yanayozidi kukua kwa kasi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Asia, Mbunge wa Manyara Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Ziwa Babati limekuwa na changamoto na magugu sambamba na maeneo mengine. Serikali tumeandaa mpango maalum hivi sasa kubainisha juhudi tulizonazo juu ya mpango huo lengo kuangalia maeneo ya changamoto mbalimbali. Kwa hiyo, tuko katika stage ya kutafuta fedha siyo Ziwa Babati peke yake lakini na maziwa mengine yanayokabiliana na magugu katika maeneo mbalimbali.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba unasafishwa, kina kinaongezwa na kingo za mto zinajengwa?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Same Jimbo la Same Mashariki kuna mito mikubwa mitatu ambayo inatitirisha maji bondeni ili wananchi watumie katika umwagiliaji wa mpunga kwenye Kata za Maore, Ndungu na ...

SPIKA: Swali?

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Tatizo hii mito imejaa magugu imejaa magogo. Je, Serikali iko tayari kusaidia mito hii isafishwe ili maji yatiririke kwa urahisi? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ni jukumu la Serikali kusaidia maeneo mbalimbali na hata eneo hilo kifupi ni kwamba niwatume wataalam wangu kwenda kuangalia kufanya need assessment ya eneo lile, lengo ni kwamba tunapoenda kutafuta mipango ya kutafuta fedha na eneo hilo tuweze kulishughulikia maana yake sambamba na Ziwa Jipe ambalo liko katika Wilaya ya Mwanga kule katika Mkoa wa Kilimanjaro.