Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 371 2022-06-10

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika mpango wa kuimarisha huduma za zimamoto na uokoaji nchini kwa kuimarisha na kuongeza vifaa vya kisasa. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 vitajengwa jumla ya vituo saba vya zimamoto na uokoaji kwa kuanza na mikoa isiyokuwa na vituo hivyo. Mikoa hiyo ni pamoja na Songwe, Simiyu, Kagera, Njombe, Manyara, Katavi na Geita. Aidha, kwa kuzingatia ukuaji wa haraka wa Jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya nchi, ujenzi wa vituo viwili Chamwino na Nzuguni utakamilika hivi karibuni.

Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa ajira mpya ya askari 400 ambao kwa sasa wapo mafunzoni. Vilevile Serikali itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu kinga dhidi ya majanga ya moto kuanzia shuleni, maeneo ya biashara na yale yenye mikusanyiko mikubwa ya watu. Nashukuru.