Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Naomba niulize swali; je Serikali haioni haja ya kurejesha huduma hii katika halmashauri sasa hivi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Wizara imejipanga vipi kudhibiti janga la moto katika masoko nchini? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza Mheshimiwa Bushiri kama kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja; kuhusu umuhimu wa kurejesha huduma hizi halmashauri, naomba nilikumbushe Bunge lako tukufu kwamba huko nyuma huduma hizi zilikuwa zinatolewa na halmashauri, baada ya kuthibitika kwamba weledi na uwezo wa halmashauri kutekeleza jambo hili ni changamoto ikaamuriwa huduma hizi zirudi Makao Makuu na ndiyo ikaimarishwa hili Jeshi la Zimamato na Ukoaji. Kwa hiyo kama tunazungumza kurejesha itabidi tufanye tathimini kujiridhisha leo ule uwezo ambao haukuwepo miaka kumi iliyopita kama umekuwepo na hivyo kuona umuhimu wa kurejesha hizi huduma.

Hata hivyo, wananchi wanao hudumiwa wapo kwenye halmashauri na wengi ni wafanyabiashara ni wazi kwamba bajeti ya zimamoto ni changamoto, hivyo halmashauri zinatakiwa kuanza kutenga bajeti kwa ajili ya kununua vifaa ili askari wetu waliopangwa kwenye maeneo hayo wavitumie vifaa hivyo kuzima moto kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, swali la pili juu ya namna ya kudhibiti majanga ya zimamoto yanayozidi kuongezeka; nakiri kwamba yapo ndiyo maana nimebainisha mikakati hapa itakayosaidia kuimarisha utoaji wa huduma za zimamoto na ukoaji ikiwa ni pamoja na mafunzo, lakini vilevile elimu kwa umma na kuzingatia weledi katika ujenzi wa majengo yetu. Nashukuru.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa changamoto ya vifaa katika Jeshi la Zimamoto ni mtihani hasa katika Manispaa ya Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, unaunguliwa mita 100 zimamoto inakuja inashindwa kuzima moto, je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya zimamoto katika Manispaa ya Shinyanga?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi ipo mikakati mingi ambayo tunaitumia katika kuboresha, moja; ni ajira kwa kuongeza nguvu kazi lakini pili manunuzi ya vifaa mmetupitishia bajeti hivi juzi zaidi ya bilioni 11 zinakwenda kununua vifaa ambavyo vitapeleka kwenye maeneo yenye changamoto kubwa ikiwemo Mkoa wa Shinyanga. Nashukuru.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii; kwa kuwa halmashauri nyingi hazina zimamoto, je, Serikali ipo tayari kujipanga upya sasa badala ya kutoka katika sehemu moja za Wilaya na Manispaa na Majiji kwenda katika Halmashauri zetu au kukasimu madaraka ya zimamoto katika Halmashauri ili kuweka wigo mpana wa namna ya kuzima moto katika maeneo yetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Massare, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyosema kwenye jibu la msingi zipo halmashauri ambazo hazina kabisa huduma hizo, lakini ipo mikoa pia ambayo haina huduma hizo, ndiyo maana tukasema kulingana na mipango yetu na bajeti tutaanza na mikoa ambayo haina kabisa huduma za zimamoto na ukoaji tukiendelea kuimarisha uwezo huo kwenye mamlaka kubwa kama manispaa, miji na majiji baadaye tutaendelea kupanua huduma hizi kwenda Mamlaka za Serikali za Mitaa ambazo zipo vijijini. Nashukuru.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante, kutokana na majanga makubwa ya Mkoa wa Dar es Salaam hasa kuunguliwa kwa masoko.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza magari ya zimamoto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kweli kwamba Jiji la Dar es Salaam linaongoza katika majanga haya ambayo tumejiridhisha kwamba mengine ni uzembe, lakini mengine ni miundombinu ambayo husababisha athari za moto. Kwa kuzingatia hilo ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu tayari tuna magari matatu yaliyokuwa yanatengenezwa na kiwanda chetu cha NYUMBU yatagawiwa kwenye mikoa yenye changamoto kubwa likiwemo Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mwaka ujao tunayo bajeti ya zaidi ya Euro milioni 4.9 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya magari na maeneo yote yenye changamoto yatagawiwa vifaa hivyo.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI K.n.y. MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuimarisha Jeshi la Zimamoto hasa katika maeneo ya miji yenye hatari kubwa ya majanga ya moto?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Mkoa wetu wa Iringa kuna msitu Mufindi, Mgololo na kuna msitu katika Wilaya ya Kilolo na moto kila wakati umekuwa ukitokea katika hiyo misitu; ni lini Serikali itaona umuhimu wa Wilaya ya Kilolo na Wilaya ya Mufindi kupatiwa gari la zimamoto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Ritta Kabati swali lake la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba maeneo ya Mufindi na Mgololo mara kadhaa hukumbwa na majanga ya moto, niombe tu uongozi wa zimamoto Mkoa wa Iringa waweze kupangilia vizuri rasilimali za magari walizonazo ili angalau gari moja liwe kwenye Wilaya ya Mufindi kuwa na ukaribu kwenye maeneo ambayo majanga hutokea zaidi. Nashukuru.