Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 372 2022-06-10

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Kazi hii ilianza tarehe 6 Juni, 2021 na inatarajiwa kukamilika Julai, 2022. Aidha, baada ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika, Serikali itatafuta fedha ili kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.