Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa tayari upembuzi yakinifu unaelekea mwisho na barabara hii kwakweli ni muhimu sana kwa wanachi wa Jimbo la Nyamagana hususani takribani kata tano za Mkuyuni, Mahina, Mhandu pamoja na Butimba; sasa Serikali ipo tayari kuhakikisha kwamba baada tu ya upembuzi yakinifu barabara hii inaanza kujengwa?

Mheshimiwa Spika, pili; barabra hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais; ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kuhakikisha ahadi za Mheshimiwa Rais zinatimizwa kwa wakati? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ni kweli ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati huo akiwa ni Makamu wa Rais na sasa ni Rais na ndiyo maana barabara hii tayari tumeshaanza kutekeleza ahadi na tayari tunaifanyia usanifu ili iweze kukamilika na tuanze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, na barabara hii kwa swali lake la pili; tunaipa uzito mkubwa sana kwa sababu ni barabara ambayo tunaamini inakuwa ndiyo barabara kama bypass kwa mtu akitokea Nyegezi kwenda Mwanza Mjini ikitokea changamoto yoyote basi hii barabara ndiyo inayoweza kutumika kwa ajili ya kuwapeleka watu katikati ya Mji wa Mwanza. Ahsante.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa fursa na mimi ningependa kujua je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Mbalizi - Mkwajuni - Makongorosi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja tayari ipo kwenye ukamilishwaji wa kufanyiwa usanifu wa kina na baada ya hapo Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami ili kuiunganisha Mkoa wa Mbeya kwa maana ya Wilaya ya Mbeya na Wilaya ya Songwe kwa Mkoa wa Songwe, ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa barabara kutoka Iringa kwenda Pawaga kupita Kihwele - Kalenga ipo kwenye kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Je, ni lini sasa Serikali itaweza kuijenga kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara iliyotajwa ipo kwenye Ilani lakini tu nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hatuwezi tukaanza barabara zote kwa mwaka mmoja. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba kadri tutakavyokuwa tunakwenda basi hii barabara itakuwa ni moja ya barabara ambazo zitajengwa kama zilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025. Ahsante. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga barabara ya Nangwa - Kisambara - Mkondoa ambayo vinaunganisha Mkoa wa Manyara na Kondoa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Samweli Hhyuma, Mbunge wa Hanang kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni kati ya barabara ambazo zipo kwenye mpango wa kuzijenga kwa kiwango cha lami, lakini ujenzi huo utategemea na upatikanaji wa fedha. Ahsante.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii; ahadi ya Mheshimiwa Rais imetolewa pia katika Manispaa ya Kigoma Ujiji ya kujenga barabara ya kilometa 10. Ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi hiyo ya Rais?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ahadi za Rais zinapewa kipaumbele na Serikali inatafuta fedha ili kukamilisha ahadi hiyo kwa kujenga hizo kilometa 10 ambazo zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais ya kujenga barabara ya Mbuyu wa Mjerumani kupitia Magara hadi Mbulu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ahadi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais ilitolewa wakati anazindua barabara ya Magara na tayari tumeshaanza kufanya usanifu kama alivyoagiza ikiwa ni maandalizi kuijenga barabara hiyo ya kutoka Mbuyu wa Mjerumani - Magara hadi Mbulu kwa kiwango cha lami.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 7

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, kutokana na ahadi ya Serikali barabara yetu ya Ubena Zomozi – Ngerengere je, lini itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Taletale Mbunge wa Morogoro Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara iliyotajwa imetengewa fedha katika bajeti hii kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mkuyuni hadi Mhandu itatekelezwa?

Supplementary Question 8

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; Mji wa Bunda uliahidiwa kujengwa kilometa 10 barabara za mjini kwa kiwango cha lami ni lini sasa zitajengwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kusaidiana na Wizara yangu pamoja na TAMISEMI tutahakikisha kwamba ahadi iliyoahidiwa inatimizwa na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kujenga zile kilometa 10 katika Mji wa Bunda. Ahsante.