Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 373 2022-06-10

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imekamilisha kufungua barabara yote kuanzia Unyoni hadi Maguu yenye urefu wa jumla ya kilometa 25 kwa kiwango cha changarawe. Aidha, jumla ya kilometa 4.22 katika eneo la Mapera zimejengwa kwa kiwango cha lami nyepesi katika sehemu korofi. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.