Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante na nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niweke kumbukumbu sawa, barabara hii ina urefu wa zaidi ya kilometa 25, lakini hizo kilometa 25 ndizo ahadi ziko kwenye Ilani ya CCM kwamba zitajengwa kwa kiwango cha lami na barabara hii ndiyo barabara pekee inayotoa wananchi wa Hagati kuja mjini ni barabara pekee hiyo hiyo tu.

Mheshimiwa Spika, swali langu nimeuliza ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara hii?

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili; barabara hii inaenda mpaka Nyasa, kwa hiyo, kule chini bado haijafunguliwa, je, Serikali iko tayari kuifungua barabara hii hadi kufika Wilaya ya Nyasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante na napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, barabara hii tunatafuta fedha ili iweze kujengwa yote kwa kiwango cha lami, lakini Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara hii inapita kwenye maeneo mengi yenye miinuko na makorofi na ndiyo maana Serikali iliona bora ianze kwanza kwa kujenga kwa kiwango cha lami yale maeneo yote ambayo ni korofi ili iendelee kupitika lakini maeneo mengine yakiwa ya changarawe.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuifikisha hii barabara hadi Nyasa naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwakuwa tunaona ni barabara muhimu kuunganisha Mbinga na Nyasa, Wizara yangu kusaidiana na wenzetu wa TAMISEMI - TARURA tutakubaliana namna ya kuhakikisha kwamba tunafungua hii barabara hadi Nyasa ili kurahisisha mawasiliano kwa wananchi hawa. Ahsante.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 2

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Simbo – Kalya kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nashon Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Simbo – Kalya ipo kwenye Ilani na Serikali inaendelea kutafuta fedha lakini kabla ya kuijenga barabara hii Serikali kwanza imeamua ijenge daraja la kudumu la Mto Malagarasi Chini na hatua ya pili itakayofuata itakuwa ni kutafuta fedha kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, mwaka 1973 Serikali ilifanya uamuzi wa kujenga Kiwanda cha Nguo cha Mbeya Textile cha pale Mbeya na lengo lilikuwa ni kwamba kiwanda hicho kitapata malighafi ya pamba kutoka katika Mikoa ya Shinyanga, Tabora na Mwanza kupitia barabara kutoka Tabora hadi Mbeya.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sababu barabara hiyo haijajengwa hadi leo, kiwanda kile kilikufa. Je, Serikali itajenga lini hiyo barabara kutoka Tabora hadi Mbeya hususan kipande cha kutoka Ipole hadi Rungwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, Mbunge wa Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Ipole – Rungwa hadi Makongolosi ni barabara kuu na ni barabara ambayo ipo kwenye mpango na imetengewa fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, kuanza kwa barabara hii kutategemea tu na fedha itakavyopatikana, lakini tayari ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuijenga barabara hii. Ahsante.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumeona kwenye vyombo vya habari, Serikali imekamilisha mazungumzo na Benki ya Dunia, hivyo kupelekea kupata fedha za ujenzi wa barabara kutoka Mtwara - Mingoyo hadi Masasi kilometa 201. Je, sasa ujenzi huo utaanza lini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chikota kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Rais katika jitihada za kufungua nchi na kuboresha usafirishaji, World Bank wako tayari kuijenga barabara ya Mingoyo hadi Masasi, barabara kuu ambayo ilikuwa kwa kweli imechakaa. Kuanza kwake kutategemea tu na jinsi taratibu za fedha kuhamisha kutoka World Bank kuja kwetu itakavyokuwa zimekamilika, barabara hii itaanza mara moja baada ya kupokea hizo fedha. Ahsante.

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 5

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Rujewa – Madibila – Kinanyambo - Mafinga ni muhimu sana kwa wananchi wa Mbarali na upembuzi yakinifu ulishafanyika; je, ni lini sasa Serikali itaanza rasmi ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Francis, Mbunge wa Mbarali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii ni barabara moja muhimu sana na ya kiuchumi na ni fupi kutoka Igawa – Rujewa kuja Mafinga. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami kwa ajili ya kuboresha usafiri kati ya Mbarali na Mafinga. Ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 6

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara ya kutoka Masumbwe – Rugunga - Ushirika kwenda kuunganishwa na Mkoa wa Geita, lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoiainisha itajengwa kadiri fedha zitakavyopatikana kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 7

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi.

Mheshimiwa Naibu Waziri barabara ya kutoka Chala - Mpalamawe ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano, pia ilikuwepo kwenye Ilani, lakini sasa hamuitamki. Nataka kujua, mna mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni barabara kuu, lakini ni barabara ambayo kwa sababu barabara nyingine ilikuwa inapita kwenye Makao Makuu ya Wilaya, Serikali iliamua kwanza ijenge barabara kupitia Makao Makuu na hii ifuate. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri Serikali itakavyopata fedha barabara hii pia itajengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Unyoni hadi Maguu?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naulizia barabara ya Kibiti kupitia Dimani kwenda Mloka kwenye Bwawa la Mkakati la Mwalimu Nyerere ni lini itajengwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Alice Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoianisha inakwenda kwenye Bwawa la Nyerere na ni barabara ambazo Wizara inaangalia uwezekano kama alivyosema Mheshimiwa Waziri ziingie kwenye mpango wa EPC+F ili kuweza kuiharakisha kuijenga barabara hii, ahsante.