Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 375 2022-06-10

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kipoza umeme transfoma kutoka kwenye umeme wa msongo wa kV 132 pale Mkata?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka wa fedha wa 2022/2023 imetenga jumla ya shilingi bilioni 16.94 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 120 kilichopo katika eneo la Mkata, Wilaya ya Handeni Vijijini. Ujenzi wa kituo hicho unatarajia kuanza mwezi Agosti, 2022 na kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kituo hiki utaenda sambamba na ujenzi wa njia ya kusambaza umeme ya msongo wa kV 33 yenye urefu wa kilometa 40 kutoka Mkata hadi Kwamsisi kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa umeme katika machimbo graphite yaliyopo katika eneo la Kwamsisi. Pia Mradi huu ni sehemu ya mradi mzima wa Kuimarisha Gridi ya Taifa (National Grid Stabilization Projects) ambao umetengewa jumla ya shilingi bilioni 500 katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha.