Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kipoza umeme transfoma kutoka kwenye umeme wa msongo wa kV 132 pale Mkata?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Spika, Jimbo letu la Handeni Vijijini lina vitongoji takribani 770; sasa ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka umeme wa REA katika vitongoji hususani vile ambavyo vina kaya nyingi? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama tulivyoeleza katika Bajeti yetu ya Wizara ya Nishati kwa mwaka ujao wa fedha Serikali imeanza program mahususi ya kupeka umeme vitongojini na tumetenga shilingi bilioni 140 kama sehemu ya maandalizi ya kazi hiyo ambayo itaongezeka kasi yake pale ambapo tutakuwa tumepata rasilimali za kutosha, lakini ni kweli kwamba baada ya kupeleka umeme katika maeneo mengi ya vijijini, maeneo ambayo yanasubiri umeme ni ya vitongoji na vitongoji hivyo katika Wilaya ya Handeni Vijijini pia vitazingatiwa katika mipango ya Serikali ya kupeleka umeme vitongojini.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kipoza umeme transfoma kutoka kwenye umeme wa msongo wa kV 132 pale Mkata?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga transfoma yenye uwezo wa MVA 90 katika substation ya Mbagala iliyoko katika Jimbo la Mbagala?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Jimbo la Mbagala ni moja ya maeneo ambayo yana mahitaji makubwa ya umeme, lakini miundombinu ni finyu, kwa hiyo kumekuwa na changamoto kubwa ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa anatuletea mara kwa mara, ya kadhia ya kukatika kwa umeme au umeme kuwa na nguvu ndogo.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpa taarifa njema Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo la Mbagala, kwamba Serikali tayari imekwisha kuagiza transfoma hiyo kubwa kwa ajili ya kufungwa katika kituo cha kupoza umeme Mbagala na kabla ya mwaka ujao wa fedha kwisha transfoma hiyo itakuwa imefungwa na kuweza kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Jimbo la Mbagala, lakini na Majimbo mengine Temeke na mkoa mzima wa Dar es salaam kwa ujumla. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kipoza umeme transfoma kutoka kwenye umeme wa msongo wa kV 132 pale Mkata?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa, Kata za Kibosho, Kilima, Kibosho Kati, na Kibosho Magharibi katika Jimbo la Moshi Vijijini lina tatizo la low voltage.

Je ni lini Serikali itatusaidia kutatua changamoto hii kwa sababu umeme uwa unawake kuanzia saa tano usiku?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa katika Mkoa wa Kilimanjaro na Wilaya ya Moshi Mjini na Moshi Vijijini kumekuwa na changamoto ya kufifia kwa umeme na nguvu ndogo ya umeme na Serikali imelibaini hilo na ndio maana imeanzisha programu kubwa kabisa ya National Grid Stabilization Project. Na maeneo haya ya Kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge yamo katika miradi ya kuimarisha Gridi ya Taifa. Kwa hiyo napenda nimpe faraja, na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatekeleza mradi wa kuimarisha upatikanaji wa umeme katika kata zake za Jimbo la Moshi Vijijini.