Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 42 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 376 2022-06-10

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Momba na lini huduma za Mahakama za Mwanzo zitaanza kutolewa katika Tarafa ya Msangano?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA aliibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Momba ni moja ya Wilaya ambazo zimepewa kipaumbele kwenye Mpango wa ujenzi wa Mahakama katika mwaka wa fedha 2023/2024 ili kuhakikisha kuwa Mahakama inakuwa na majengo yake yenyewe na mazuri.

Mheshimiwa Spika, vilevile, ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo ya Tarafa ya Msangano umepangwa kufanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023 ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya mahitaji kama watumishi ili huduma zitolewe mara baada ya ujenzi kukamilika.