Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 378 2022-06-13

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti wa Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018, 2018/2019 na 2019/2020 Serikali ilipeleka jumla ya shilingi milioni 835.95 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi mpya ya mabasi katika eneo la Kyakailabwa Kata ya Nyanga. Fedha hizo zilitumika kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kuingilia stendi kwa kiwango cha lami, ujenzi wa vyoo, ujenzi wa mabanda matatu ya abiria na kituo cha polisi umekamilika. Aidha, ujenzi wa eneo la maegesho ya mabasi na malori upo hatua ya changarawe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 imejumuisha mradi wa stendi hiyo kwenye Mpango wa TACTIC awamu ya pili. Ahsante.