Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Kwa vile Serikali ilishaahidi kutoa bilioni moja kuanzia Julai na tunaamini itakuja; je, sasa Manispaa ya Bukoba Mjini ianze kutangaza tender kama TARURA wanavyofanya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili kwa kuwa stendi ya Bukoba Mjini imewekwa katika miradi ya TACTIC, naomba kujua utekelezaji wa mradi huu utaanza lini katika Manispaa ya Bukoba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Semuguruka kwa namna ambavyo anashirikiana kwa karibu sana na Mheshimiwa Mbunge Stephen Byabato, Mbunge wa Bukoba Mjini kuhakikisha miradi inakwenda vizuri, lakini nimuhakikishie kwamba suala la ahadi ya Serikali ya bilioni moja ni ahadi ya Serikali na tutahakikisha fedha hiyo inakwenda mwaka wa fedha ujao tunaoanza Julai ili kazi zianze. Lakini ni vema tusubiri fedha ziingie ndipo tuanze kutangaza zabuni kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili kuhusiana mradi wa TACTIC unaoanza awamu ya pili mwaka wa fedha baada ya 2022/2023. Ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Mkoa wetu wa Iringa kuna stendi ile ya Igumbilo tunashukuru, lakini stendi ile iko mbali sana na wananchi imekuwa ni mateso wananchi wamekuwa wakifika usiku sana wanapigwa na wajambazi.

Je, hivi ni kanuni au sheria kwamba haya mabasi yasishushe abiria katika stendii za zamani kwa sababu wananchi wengi wengi wanapata mateso makubwa sana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali siku zote ni kuboresha huduma za wananchi, lakini pia kurahisisha Maisha ya wananchi katika maeneo yao. Kwa hiyo naagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa lakini na menejimenti nzima ya Mkoa wa Iringa kufanya tathimini ya athari ambazo zinatokana na kuacha kutumia stendi ya zamani na kutumia stendi mpya peke yake na kuona busara inaongoza nini ili wananchi wapunguziwe adha ya usafiri. Ahsante sana.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais alipopita Lamadi Wilaya ya Busega aliahidi ujenzi wa stendi, je, ni lini utaanza ujenzi huo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi za viongozi wetu ni maelekezo kwa Wizara na mimi nimhakikishie kwamba tumeshapokea maelekezo hayo tunachofanya sasa tunatafuta fedha, lakini tunafanya usanifu kwa ajili ya kutafuta fedha, lakini tunafanya usanifu kwa ajili ya kuanza kujenga stendi ya mabasi ya Busega baada ya kupata fedha kwa ajili ya shughuli hiyo. Ahsante sana.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe stendi ya Mkoa iko Njombe na kwa sababu Njombe ni pembezoni mwa mji, unapozungumzia mji ni Makambako ambako ndiyo highway ya kwenda Malawi kwenda Songea, kwenda Mbeya na kadhalika. Ni lini sasa stendi ya mabasi ya Mji wa Makambako itajengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga almaarufu Jah People, Mwenyekiti wetu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, stendi ya Mkoa wa Njombe ni kweli iko katika mji wa Njombe, lakini naomba tukubaliane kwamba tunaichukua hoja hii ya Mheshimiwa Deo Sanga, nafahamu Makambako pale tuna stendi, lakini ni stendi ya mji inayohitaji maboresho kwa hiyo tutakaa mimi na Mheshimiwa Sanga tukubaliane tuone Wizara inaweza ikafanya nini kuboresha stendi pale Makambako Mjini. Ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kuweza kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mbea ni miongoni mwa majiji makubwa katika nchi yetu ya Tanzania, lakini mapka sasa hatuna stendi yenye hadhi ya jiji.

Je, ni lini sasa Serikali itajenga stendi yenye hadhi ya jiji kwenye mkoa wetu wa Mbeya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Jiji la Mbeya ni jiji kubwa, lakini bado tunachangamoto ya stendi inayofanana na hadhi ya Jiji la Mbeya, lakini nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Tulia Ackson, Mbunge wa Mbeya Mjini pia amekuwa akifuatilia sana suala hilo nakushukuru sana kwa kumuunga mkono, lakini Serikali inafanya tathimini na tumeshaelekeza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuleta andiko la mapendekezo ya kujenga stendi ili tuone kama wanaweza kujenga kwa mapato ya ndani au kama mradi wa kimkakati ili Serikali tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi huo. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kujenga stendi ya mikoani katika Jimbo la Mbagala hasa Mikoa ya Kusini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Chaurembo, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la Mbagala ni eneo ambalo wananchi wengi wa Mikoa ya Kusini wanatumia kama sehemu ya kufikia au kuanza safari kuelekea mikoa ya Kusini, kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Mbunge lakini niagize Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kufanya tathimini ya uwezekano wa kutekeleza mradi huu kwa maana ya kupata eneo, lakini pia kufanya makadirio ya gharama ili tuweze kuona kama Serikali nini kinaweza kikafanyika. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 7

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kuwa Mji wa Namtumbo ni mji ambao unapita mabasi yanayokwenda Masasi, Mtwara, Lindi mpaka Dar es Salaam kwenda kwenye Kituo cha Mbagala, lakini hatuna stendi ya mabasi na halmashauri yetu haina uwezo wa kujenga stendi ya mabasi lakini uwanja upo. Je, Serikali ipo tayari kututengea fedha kujenga stendi ya mabasi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Jimbo na Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe maelezo ya ujumla kwa wakurugenzi wote wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa walishapewa maelekezo kuainisha vipaumbele vya miradi yenye tija kwa jamii zikiwemo stendi, kwa hiyo ni hoja ya msingi kwamba Wakurugenzi akiwepo Mkurugenzi wa Namtumbo walete makadirio ya ujenzi wa stendi hiyo ili Serikali ione namna gani inaweza ikatekeleza mradi huo. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 8

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Wilaya ya Lushoto hasa Lushoto Mjini stendi yake ni yazamani sana. Je, Serikali inampango gani wa kujenga stendi mpya sasa Wilayani Lushoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe halmashauri ya Lushoto na Mheshimiwa Mbunge kushirikiana nao kama sehemu ya Baraza la Madiwani kutuletea mapendekezo yao, lakini na tathimini ya gharama ili sasa Serikali iweze kuona utaratibu ambao utatumika kujenga stendi hiyo kwa sababu ni mahitaji ya wananchi. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi kuu ya mabasi Bukoba Mjini?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona; je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya eneo la Madira kule Jimbo Arumeru Mashariki ambao mradi huu ulisitishwa katika hatua za mwisho katika utekeleza mwaka 2019?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ndiyo nimepata taarifa hii kwamba huo mradi umekwama naomba nilichukue hili baada ya session hii ya maswali na majibu nikae na Mheshimiwa Dkt. Pallangyo tujuwe hiyo stendi kwa nini imekwama na sisi tutatumia wataalamu wa Wizara kufanya tathimini lakini kukwamua mkwamo ambao hupo katika stendi hiyo. Ahsante.