Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 380 2022-06-13

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na matukio ya uhalifu ukiwemo wizi katika Jimbo la Pangawe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Amour Haji, Mbunge wa Pangawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itaendelea na kazi ya kulinda maisha ya watu na mali zao kwa kufanya doria, kuendesha operesheni mbalimbali na misako ili kuwabaini na kuwakamata wahalifu. Jeshi la Polisi limewapanga Wakaguzi wa Polisi kila Shehia katika Jimbo la Pangawe ili kusimamia usalama na kuishirikisha jamii kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, uhalifu ni zao la jamii, hivyo naomba kutumia nafasi hii kuwaomba wazazi, walezi, viongozi wa dini na jamii kwa ujumla kuwalea kwa maadili mema vijana wetu ili waepuke kujiingiza katika uhalifu. Aidha, watumie fursa za uwezeshaji wananchi kiuchumi zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa wale watakaokaidi wajiandae kukabiliana na mkono wa sheria. Nashukuru.