Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na matukio ya uhalifu ukiwemo wizi katika Jimbo la Pangawe?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza nashukuru kwa jibu lake zuri Mheshimiwa Naibu Waziri, pia nina swali langu la nyongeza.

Katika Jimbo langu la Pangawe kuna kituo kidogo cha polisi kinaitwa Kijitopele. Bahati nzuri kwamba au bahati mbaya kunakuwa na wahalifu wengi sana ambao wanakitumia kituo kile na ukiangalia wahalifu wale maana yake wanakuwa hawana nafasi ya kutosha ndani ya kituo kile. Je, Serikali ina mpango gani kukiboresha Kituo cha Kijitopele? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Haji Amour Haji, Mbunge wa Pangawe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishasema katika nyakati tofauti na bahati nzuri kwa Zanzibar nimeshatembelea vituo hivyo na kubaini kwamba vingine vina hali dhaifu, tutaendelea kupitia Mfuko wa Tuzo na Tozo kuviimarisha vituo hivi na kuwapanga askari watakaotoka vyuoni ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kikiwemo hiki kituo alichokitaja Mheshimiwa Mbunge wa Pangawe. Nashukuru.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na matukio ya uhalifu ukiwemo wizi katika Jimbo la Pangawe?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumezuka vikundi vya wahalifu katika Kata ya Makulu, Jiji la Dodoma vinavyojiita panya karowa. Nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha kwamba vikundi hivi haviendelei katika maeneo mengine na kuleta uhalifu? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tunapiga vita makundi yote ya wahalifu awe mtu mmoja au vikundi kama ilivyokuwa panya road Dar es Salaam. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa Dodoma hiyo kazi pia imeanza na baadhi ya vijana wa aina hiyo wameshatiwa nguvuni. Sasa hilo ulilosema eneo gani umetaja Kata ya hawa panya nini karoga? Tutashughulika nao hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kikao hiki tutaongea na Mbunge ili anieleze kwa ufasaha ni eneo gani na kundi hili ili askari wetu wa Jiji la Dodoma waweze kushughulika nao. Nashukuru. (Makofi)

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na matukio ya uhalifu ukiwemo wizi katika Jimbo la Pangawe?

Supplementary Question 3

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la uhalifu limekuwa likiongezeka siku hadi siku katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar na tatizo hili limeshazungumzwa sana hapa Bungeni.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mkakati gani wa kushirikiana na Vikosi Maalum vya SMZ kule Zanzibar ili kuweza kutokomeza na kufanya jambo hili kuwa historia? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed - Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, makosa ya uhalifu kama ambavyo yanatokea maeneo tofauti, yamebainishwa Zanzibar vikundi vinaongezeka na nilikuwepo kule, viko vikundi vingine vya wavuta bangi. Lakini kinachofurahisha Jeshi la Polisi Kamisheni ya Zanzibar wanafanya kazi nzuri sana na kwa kawaida vyombo hivi hushirikiana na vyombo vingine vya usalama vikiwemo SMZ katika vikao mbalimbali vya ngazi ya Mkoa, kuna Kamati za Usalama za Mkoa, ngazi ya Wilaya kuna Kamati za Usalama za Wilaya na hivyo kupeana ushauri na mbinu za kukabiliana na matukio haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikuhakikishie polisi wetu wako imara kwa kushirikiana na vyombo vingine watakabiri makundi haya yanayoibukia huko Zanzibar kwa madhumuni ya kuyadhibiti. Nashukuru.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na matukio ya uhalifu ukiwemo wizi katika Jimbo la Pangawe?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru; ukatili katika jamii kama ambavyo umeibuka ukatili wa wahalifu wa panya road, kumeibuka ukatili mkubwa sana kwa wanawake na watoto hasa kipindi hiki wanawake wanauliwa, watoto wanafanyiwa vitendo vya ajabu, lakini bado hatujaona jitihada za dhati za Serikali kupitia Jeshi la Polisi kukabiliana na uhalifu huu wa kuwadhuru wanawake na watoto ambao wanatakiwa walelewe vizuri, wawe watumishi bora huko baadae? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yapo matukio mengi yanaripotiwa ya uhalifu yanayohusisha mauaji, lakini na mateso kwa watoto, kwa wanawake lakini wakati mwingine hata kwa wanaume. Mimi niseme kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, uhalifu ni zao la jamii. Ipo haja ya wazazi, walezi, watu wa dini, viongozi kama sisi kwa pamoja tushirikiane kukabiliana na uhalifu huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Jeshi la Polisi kila inapotokea kupata taarifa ya uhalifu huu, huchukua hatua bila kumchelea mtu. Kwa hiyo, niahidi tu Mheshimiwa Bulaya tutaendelea kushirikiana na wadau wa amani kokote walipo ili kudhibiti matendo ya namna hii kwenye jamii zetu. Nakushukuru sana.