Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 382 2022-06-13

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika uchumi unaozingatia misingi ya Sera ya soko huria ujenzi wa viwanda mbalimbali vikiwemo viwanda vya kuchakata samaki unafanywa na sekta binafsi. Jukumu la Serikali ni kuweka mazingira wezeshi na rafiki ya uwekezaji kwenye sekta ya viwanda. Kwa kuzingatia sera hiyo Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na kuhamasisha wawekezaji mbalimbali wa ndani na nje kuja kujenga viwanda vya kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe pamoja na maghala ya kuhifadhia na kugandisha mazao ya uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuhamasisha sekta binafsi kujenga viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi, maghala ya kuhifadhia na kugandishia mazao ya uvuvi katika maeneo ya uvuvi yenye mavuno mengi hapa nchini ikiwemo Wilaya ya Ukerewe. (Makofi)