Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa bado uhamasishaji unaendelea, lakini wavuvi wetu wengi hawa wadogo wanakosa elimu na zana kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao, lakini vilevile wanakosa taarifa za kutosha za masoko yanayoweza ku-determine bei ya bidhaa zao wanazozalisha. (Makofi)

Nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wanasaidia jamii hii hasa kwenye eneo la Ukerewe ili wavuvi wetu waweze kunufaika na shughuli zao za uvuvi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuzingatia mazingira ya Ukerewe kama eneo maalum la uvuvi; nini sasa mkakati wa kujenga mwalo kwenye eneo la Kakukuru kwenye Wilaya yetu ya Ukerewe? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili kwa pamoja ya Mheshimiwa Joseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango mkakati wa namna ya kuwasaidia wavuvi wetu hapa nchini ili kuwasaidia wawe na zana bora, lakini pia waweze kuongeza uzalishaji wa mazao ya samaki hapa nchini. Mojawapo ya mkakati ni kwenye bajeti ya mwaka ujao tuna mpango wa kununua boti 320 kwa nchi nzima ili tuweze kuzikopesha kwa wavuvi wadogo wadogo na wavuvi wa kati waweze kuwa na uwezo wa kuvua katika maji marefu upande wa bahari, lakini pia upande wa maziwa yetu. Lakini pia tuna mpango wa kuboresha mialo yetu yote na kuijenga katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuboresha masoko madogo madogo ya wavuvi wetu kwa kujenga vichanja ili mazao yale yanayotolewa baharini au ziwani yaweze kupata mahali pa kuanikwa vizuri, lakini yaweze kuwa bora na kuweza kupata bei iliyo nzuri kwenye soko letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala lake la pili, Serikali imepanga kukarabati mwalo wa Kakukuru kwenye Wilaya ya Ukerewe ili kwamba mwalo ule uwe bora, ili kwamba wavuvi wa Wilaya ya Ukerewe wapate mahali ambapo wanaweza wakashusha mavuvi yao vizuri na kwa urahisi zaidi. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru kunipa nafasi.

Mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi ni mikoa ambayo inamiliki Ziwa Tanganyika, kwa bahati mbaya sana mikoa hii yote hakuna sehemu Serikali imewekeza viwanda vya kuchakata samaki.

Ni lini Serikali itapeleka viwanda kwenye maeneo ya mikoa hiyo ili kuepukana na wizi unaofanywa na nchi jirani kwenye maeneo ya kwetu? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa sasa imefaulu kumpata mwekezaji ambaye amejenga kiwanda cha kuchakata mazao ya uvuvi kwenye Mji wa Sumbawanga. Kiwanda hiki hivi karibuni kitaanza uchakataji wa mazao ya uvuvi, lakini pia Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji kutoka sekta binafsi ili pia kuwekeza kwenye maeneo ya ukanda mzima wa Ziwa Tanganyika kuanzia Kigoma kuja Mkoa wa Katavi mpaka Rukwa.

Kwa hiyo, Serikali tunaendelea na uhamasishaji na wawekezaji wakipatikana tutawapeleka kwenye ukanda wa Ziwa Tanganyika ili waweze kuwekeza zaidi. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 3

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza; kwa kuwa mnada wa Upili wa Olokii miundombinu yake imeharibika sana, mizani imekufa, hakuna maji na Wizara ndio inakusanya fedha zote katika mnada huo wa Upili.

Ni lini Serikali itakarabati mnada huo ili kuhakikisha kwamba huduma nzuri na bora inapatikana kwenye mnada huo wa Olokii? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Serikali kwenye bajeti ya mwaka ujao imetenga shilingi bilioni 21.2 kwa ajili ya kukarabati minada yake ya Upili na minada ya mipakani yote, ili kuweza kuwarahisishia wafugaji ambao wanapeleka mifugo yao kwenye minada hiyo. Kwa hiyo, miongoni mwa mnada ambao Mheshimiwa Mbunge anausema utafanyiwa ukarabati kupitia bajeti hii. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Waziri mwaka jana ulikuja Kirando na ukaona kwamba ule mwalo uliokuwa umewekwa na Serikali umezama. Nini mpango wa Serikali wa kujenga soko ambalo nilikuonesha kwamba eneo tayari tumeliandaa pale Kirando? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nilifika Kirando na kweli mwalo ule tuliukarabati na kujenga miundombinu mbalimbali lakini umezama. Lakini ahadi yetu Mheshimiwa Mbunge iko pale pale kwamba tutaujenga upya Mwalo wa Kirando kwa kutumia bajeti ambayo tayari tumetengewa na Serikali, ili kuhakikisha kwamba ubora tuliokuwa tunautaka utokee kwenye mwalo huo unaendelea kuwepo.

Kwa hiyo, tutaendelea na juhudi kwa mwaka wa fedha ujao kuweza kukarabati miundombinu iliyoko hapo, ili pia kuweza kuwasaidia wavuvi wetu hasa eneo la Kirando ambao wanavua kwa wingi sana. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; Mkoa wa Mara ulikuwa na viwanda vinne vya kuchakata Samaki, lakini vyote vimekufa kimebaki kimoja tu cha Musoma Fishing Process kwa sababu ya changamoto mbalimbali ikiwepo ukosefu wa miundombinu rafiki wa uwanja wa ndege ambao ungeweza kusafirisha mazao ya samaki kwenda nje na sasa tunasafirisha malighafi kwenda Nairobi ili yaweze kuchakatwa yatoke nje.

Sasa ningetaka kujua mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba inatatua changamoto mbalimbali ili viwanda vyetu vile vifufuliwe na kuweza kuuza mazao ya samaki na sio malighafi ya samaki? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, ni kweli kwamba viwanda vilikuwepo kwenye Mji wa Musoma na ukanda wote wa Ziwa Tanganyika upande wa Mkoa wa Mara na sasa kiwanda kimoja kinaendelea kufanyakazi. Lakini nitoe tu ufafanuzi kwamba viwanda vingi pia havifanyikazi kwa sababu ya matatizo ya kiuendeshaji, matatizo ya kimenejimenti ya wenye viwanda wenyewe. Sababu sio moja tu kwamba miundombinu inayohusiana na kuongeza masoko na kadhalika ndio inayosababisha hiyo. Viwanda vingi vya wawekezaji hasa vya samaki vimekumbwa na tatizo la uendeshaji wa viwanda hivyo, matatizo ya kimenejimenti. Kwa hiyo, Serikali kama Serikali tuko tunazungumza nao na kuona ni kwa namna gani viwanda vile vinaweza vikafufuliwa au basi kuvikabidhi kwa wawekezaji wengine binafsi ili viweze kuendelea kufanyakazi. Kwa sababu…

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 6

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itajenga chanja za kuanika dagaa Kanda ya Ziwa ili wafanyabiashara hasa akinamama walioko kule waweze kupata masoko lakini pia waweze kupata faida katika biashara zao wanazozifanya? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana mwaka wa fedha ujao unaoanza tarehe 1 Julai, Wizara na Serikali kwa ujumla tumekubaliana na Benki ya Wakulima – TADB kutoa mikopo kwa wavuvi na kwa wafugaji. Kwa hiyo, ninaamini Mheshimiwa Furaha atahamasisha wananchi na hasa wanawake katika Mji wa Mwanza ili waweze kujitokeza na kupata fursa hii ambayo wavuvi wote wanayo katika nchi yetu, lakini pia wavuvi ambao watakuwa wako kwenye vikundi na wale wavuvi ambao watakuwa wanaweza kufanya shughuli hii binafsi binafsi. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 7

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua mpango na kazi kubwa ya Serikali ni pamoja na kuweka mazingira mazuri na mazingira wezeshi kwa wavuvi hasa kuimarisha masoko kwa sababu baada ya bidhaa kupatikana ndio ukuaji wa viwanda kwenye maeneo mengine.

Nilitaka nijue Mpango Mkakati wa Serikali mlionao kushughulikia na kukimbilia soko la mpakani kati ya Tanzania na Kenya kuweka soko pale la samaki kwa ajili ya maboresho na ukuaji wa viwanda hivyo ambavyo vinazungumzwa vya Musoma. Nataka nijue Mpango Mkakati wa Serikali mlionao. (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, nimshukuru sana Mheshimiwa Chege kwa ufuatiliaji wake hasa kuhusiana na masoko ya mazao ya uvuvi kuelekea kwenye nchi jirani ya Kenya. Tumeliona tatizo hilo na tuna mpango sasa wa kuweka utaratibu hasa kwenye mpaka ule wa Sirari ili kwamba wavuvi wanapopeleka mazao yao kwenda nchi ya Kenya au mpakani wasipate usumbufu ambao walikuwa wakiupata huko nyuma. Kwa sasa tutaweka utaratibu ambao utawasaidia wavuvi hawa kulipa tozo mbalimbali ambazo wanatakiwa kulipa za halmashauri lakini pia za Serikali Kuu, kwa urahisi zaidi ili waweze kulipata soko la nchi jirani ya Kenya ambalo mara nyingi kwa kweli linawapa bei iliyo nzuri.

Kwa hiyo, tutashirikiana na wenzetu walioko pale mpakani upande wa Wizara nyingine Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (Uhamiaji) ili kuweka urahisi utakaowafanya wavuvi wetu waweze kulipata soko la nchi jirani kwa urahisi zaidi. Ahsante sana. (Makofi)