Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 385 2022-06-13

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI K.n.y. MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaajiri vibarua wapatao 20 ambao wamefanya kazi Shirika la Reli Mkoa wa Katavi kwa miaka mitano?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mchango uliofanywa na vijana wa Kitanzania ambao wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya reli ikiwemo ukarabati wa njia ya reli katika Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania inaendelea kuwatumia vijana hao katika miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa njia ya reli na imekuwa ikiwahimiza vijana hao kujiendeleza ili kuwa na sifa ya kuajiriwa katika utumishi wa umma kwa kuzingatia Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma. Kupitia utaratibu huo vibarua wawili wamejiendeleza na kuajiriwa na wengine wanaendelea kuhamasishwa.