Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 386 2022-06-13

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeendelea kuinua tuta la barabara eneo la Kyabalamba kwa kifusi cha mawe na kujenga madaraja madogo manne. Hadi sasa tuta la mita 400 na madaraja mawili yamekamilika na kazi itaendelea mwaka wa fedha wa 2022/2023. Ahsante.