Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi ambayo imetajwa kufanyika lakini katika mvua za masika ambazo zimenyesha na kumalizika juzi hili eneo lilibomoka maji yakafurika na magari yakashindwa kupita.

Sasa swali langu liko hivi bila shaka huyu mkandarasi aliyefanya kazi hiyo alilipwa; je, Serikali ilijiridhisha kabla ya kumlipa mkandarasi kwa kazi aliyofanya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; eneo hili ni eneo la Tingatinga na ni la miaka mingi, je, Serikali haioni haja kwamba panastahili kufanyika upembuzi yakinifu makini na kwa kutumia wataalamu makini ili eneo hili liweze kutengenezwa kwa ufanisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kufanya malipo yoyote lazima Serikali ijiridhishe kwamba kazi iliyofanyika inahitaji malipo. Lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi cha mvua hata nyumba kama hii inaweza ikaondolewa na mvua. Kwa hiyo, suala la mvua ni suala lingine, lakini nachotaka kumwakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tathmini ilifanyika na kazi ilikuwa imefanyika lakini mvua inaponyesha haiwezi ikaondoa kitu chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kwa kuwa tathmini ilifanyika na eneo tunalojenga tuta walishafanya tathmini. Kwa hiyo tuna uhakika kwamba tutaendelea kuliinua hilo tuta na ndio maana tunaongeza madaraja na kuinua tuta ili eneo hilo ambalo Mheshimiwa Mbunge anafahamu ni swamp area tuta lazima liinuliwe na ndio maana tumeongeza madaraja ili yaweze kupitisha maji yasiweze kukwama, ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mbeya kwenda mpaka Dar es Salaam eneo la changarawe maarufu kama Jinja wakati wote limekuwa likisababisha ajali na kuuwa Watanzania walio wengi; na hivi majuzi Watanzania takribani 20 walifariki. Serikali ina mkakati gani kufanya tathmini hata ikibidi matengenezo kuhakikisha kwamba eneo lile haliendelei kuchukua roho za watu ambao hawana hatia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kutoa pole kwa wananchi wengi ambao siku za karibuni tumesikia wamepoteza maisha katika eneo hilo la Majinja katika Wilaya ya Mufindi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ukweli kwamba eneo hili limeendelea kusababisha ajali nyingi Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imeshawaagiza makao makuu TANROADS pamoja na TANROADS Mkoa wa Iringa kuunda timu ambayo itakwenda kufanya study kujua tatizo ni nini ambalo limeendelea kusababisha ajali katika eneo hilo, ili kama ni suala la utaalamu kwa maana ya miundombinu ya barabara timu hiyo iweze kuishauri Serikali nini kifanyike ili kuondokana na ajali kama zinasababishwa na namna yoyote ya barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa hatua za haraka tumewaagiza TANROADS Mkoa wa Iringa waweze kuweka alama nyingi za kutoa tahadhari kwamba eneo hili ni hatari ikiwa ni kuona pia uwezekano kama wanaweza kuongeza matuta ili kupunguza ajali ikiwa hiyo ni hatua za muda mfupi, ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; barabara inayotoka Ntobo - Busangi mpaka Didia kwa muda mrefu imekuwa haina matengenezo. Sasa nilitaka kufahamu ni lini Serikali itaweza kuweka matengenezo ya kudumu kwenye barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja imetengewa fedha kwa mwaka wa fedha unaokuja kwa ajili ya matengenezo ya barabara hiyo kwa mwaka huo unaokuja. Kwa hiyo, nina hakika katika mwaka unaokuja barabara hiyo itatengenezwa na tutahakikisha kwamba pengine yale maeneo yote ambayo hayapitiki ndio yanayopewa kipaumbele katika matengenezo hayo. Ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona; Serikali ilianzisha mchakato wa kujenga daraja jipya la Kikafu, na tayari kwa muda mrefu sana ilifanya tathmini kwa wananchi kupisha maeneo yao ili daraja hilo liweze kujengwa.

Swali langu ni lini Serikali italipa fidia wananchi wale waliofanyiwa tathmini na kuanza ujenzi wa daraja la kikafu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo anaitaja daraja liko kwenye barabara kuu ya Arusha - Moshi kwenda Holili, na daraja hili lipo kwenye mpango katika bajeti ambayo tumeshaipitisha. Kabla ya kuanza ujenzi naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipaumbele kitakuwa ni kwanza kuwalipa wananchi ambao wanapisha daraja hili kwa sababu tunalihamisha kabisa lilipokuwa na kulipeleka sehemu nyingine, ahsante.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, kuna juhudi gani za kufanya matengenezo ya kudumu katika eneo la Kyabalamba lililopo kati ya Kata za Rubale na Izimbya – Bukoba?

Supplementary Question 5

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona, barabara ya kutoka Dar es Salaam hadi Mbeya eneo la Mlima Kitonga limekuwa na ajali nyingi na mara nyingi kuziba barabara hiyo na kusimamisha shughuli za kiuchumi kwenye nchi yetu. (Makofi)

Ni lini sasa Serikali itafanya utaratibu au kuipanua barabara ile au kuangalia njia mbadala ili shughuli za kiuchumi zisisimame wakati kunapotokea ajali kwenye eneo lile?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli eneo la Kitonga ni eneo lenye barabara ambayo ina miinuko na kona kali na Serikali imeendelea kulifanyia matengenezo ikiwa ni pamoja na kujenga zege, kuondoa kona na kuipanua ile barabara ili kuhakikisha kwamba magari mengi na hasa ambayo ni malori yanapishana kwa urahisi.

Suala lingine ambalo sasa tunafikiria ni kuimarisha barabara ambayo ni ya bypass ili kunapotokea changamoto na barabara ikiziba basi magari hayo yaweze kupita njia ya bypass, ahsante.