Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 387 2022-06-14

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Tlemai Awack, Mbunge wa Jimbo Karatu, kama ifuatvyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 barabara NBC - Kudu yenye urefu wa kilometa 0.6 ilijengwa kwa gharama ya shilingi milioni 350. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, ujenzi wa barabara za Tarafa - Ari Mpya, TRA - Mahakamani na NBC - Kudu zenye urefu wa kilometa 0.9 kwa gharama ya shilingi milioni 499.99 ambapo hadi sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 78 na zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Canivo - Buchani kilometa 0.53; Posta - Maliasili kilometa 0.10 na Bambras - Continental kilometa 0.100 zenye jumla ya urefu wa kilometa 0.73 zinaendelea kutekelezwa ambapo hadi sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 70. Kwa upande wa mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya shilingi milioni 500 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara kilometa 0.62 kwa kiwango cha lami kwa barabara za Gorwa, Posta – Mailimbili, Bampras Continental na Rhotia Pharmacy. Serikali itaendelea kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara za Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha.