Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL T. AWACK: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa ahadi hii ya kilometa kumi ni toka Rais wa Awamu ya Nne, na leo tuko na Rais wa Awamu ya Sita; je, ni lini ahadi hii ya kilometa kumi itatekelezeka?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Mji wa Karatu uko center ya mji wa kiutalii, kati ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Lake Manyara, National Park na hifadhi ya Serengeti. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kujenga kilometa kumi ili kuimarisha mji uwe wa kiutalii katika Mji wa Karatu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Awack, Mbunge wa Jimbo la Karatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba Serikali tutaendelea kutenga fedha kila mwaka kuhakikisha ahadi za viongozi wetu wakuu ambazo walizotoa zinatekelezeka katika Jimbo la Karatu. Serikali inaona haja muhimu kabisa ya kuhakikisha kwamba barabara hizo zinakamilika kwa sababu ya umuhimu wa eneo la Karatu hususan katika sekta ya utalii.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, katika Mji wa Mbalizi, kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais wa kujenga barabara za mitaa kwa kiwango cha lami; je, ni lini barabara hizo zitajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika mchakato wa kutafuta fedha, na mara utakapopata fedha hizo maana yake tutaanza ujenzi ili kukamilisha ahadi za viongozi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeahidi kujenga barabara kilometa tano kwenye Mji wa Hyadom; je, ni lini Serikali watatimiza ahadi ya kujenga kilometa hizi za lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua ahadi ambazo viongozi wametoa ikiwemo katika eneo la Hyadom, katika Jimbo la Mbulu Vijijini ambako hadi sasa tunatafuta fedha na tumeendelea kutenga kila mwaka hizo fedha ambapo tutakuwa tunapeleka katika maeneo hayo ili kukamilisha ahadi hizo.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Supplementary Question 4

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Mji wa Nkwenda ni moja kati ya miji ambayo iliahidiwa kujengewa kilometa tano za lami, hata hivyo kilometa tano hazikujengwa ndani ya mji zilijengwa katika barabara ya TANROADS ambayo inapita nje ya mji.

Sasa nataka kujua ni lini kilometa tano zilizoahidiwa kujengwa katika barabara za ndani ya Mji wa Nkwenda zitajengwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua ahadi za viongozi hususan katika maeneo yote ikiwemo eneo la Kwera ambalo umeliainisha hapa Nkwenda na kwa hili ambalo amelieleza ni kwamba Serikali itaendelea kutekeleza kadri ambavyo tutapata fedha, ahsante.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara za ndani za kilometa 10 katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Supplementary Question 5

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, naomba kuiuliza Serikali; ni lini kilometa tano zilizoahidiwa na Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano katika Mji wa Nguruka zitajengwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nashon Bidyanguze, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa ahadi zote za viongozi tumeshazichukua pale Ofisi ya Rais – TAMISEMI na jukumu letu la sasa ni kuzitafutia fedha ili kuhakikisha kwamba zinaanza kutekelezeka.