Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 388 2022-06-14

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: -

Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi wa DMDP Awamu ya Kwanza inajenga mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 48.243 kwa gharama ya shilingi billion 60.9 katika Jimbo la Temeke kwa Kata za Mtoni kilometa 9.623; Makangarawe kilometa 10.402; Yombo vituka kilometa 7.710; Kilakala kilometa 10.53; Keko kilometa 0.462; Buza kilometa 1.7; na Kata za Changombe, Sandali, Temeke na Azimio zimejengwa kilometa 7.8. Kwa sasa kilometa 46.543 zimekamilika na zinatumika na kilometa 1.7 za Buza zilizosalia zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Septemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kupitia Mradi wa DMDP Awamu ya Pili katika Jimbo la Temeke imependekezwa kujengwa mtandao wa barabara wa jumla ya kilometa 53.10 kwa kiwango cha lami zinazokadiriwa kugharimu shilingi billioni 69.5. Ofisi ya Rais – TAMISEMI imewasilisha mapendekezo hayo Wizara ya Fedha na Mipango ili iwe sehemu ya mzunguko wa 20 wa mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia katika Mkoa wa Dar es Salaam unaotarajia kuanza mwezi Julai, 2022.