Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa kuwa Jimbo letu la Temeke limepata kilometa 53.10; je, huoni haja ya Serikali kufanya mazungumzo na Benki ya Dunia mapema ili kweli Julai hii hizo barabara zianze kujengwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa katika jibu lako la msingi umenijibu kwamba kuna kata ambazo tayari zimeshafanyiwa ukarabati na barabara hizo zinatumika. Niombe kusema kwamba katika Kata ya Chang’ombe, Sambali, Keko, Azimio, Temeke 14 na Miburani sijapata kuona hizo barabara.

Je, uko tayari kuandamana na mimi twende tukazione hizo barabara katika jibu lako la msingi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mapendekezo hayo yameshapelekwa na yapo Wizara ya Fedha, na mazungumzo yanaendelea, ni imani yangu kwamba haya mazungumzo yataisha kama ambavyo tulikubaliana mwezi wa saba ili sasa huu mradi wa kwa Halmashauri ya Temeke na Jiji la Dar es Salaam uweze kufanya kazi. Nimhakikishie niko tayari tunaweza tukaongoza na yeye siku ya Jumamosi, weekend hii kwenda kuziona barabara hizo.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuwa Jimbo la Temeke linapakana na Jimbo la Ukonga na sisi ni wanufaikaji wa mradi kwenye Kata za Ukonga na Gongolamboto.

Naomba sasa kujua nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mradi huu kwa awamu ya tatu unazinufaisha Kata za Majoe, Kivule, Kitunda na Chanika katika barabara za Pugu, Majohe – Gwera katika barabara ya Kitunda, Kivule, Msongola…

SPIKA: Mheshimiwa Jerry Silaa hilo ni swali la nyongeza unataka kumaliza barabara zote kweli? (Kicheko)

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, aondoe shaka, kuhusu utekelezaji wa mradi huu kwa kuwa ni mradi unaohusu jiji zima la Dar es Saalam ikiwemo katika Jimbolake la Ukonga. Kwa hiyo mara utakapokamilika barabara alizozianisha ziko katika huo mpango, ahsante sana.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Supplementary Question 3

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, Mji wa Mafinga ni miongoni mwa miji 45 itakayonufaika na mradi wa TACTIC ambayo pia Jiji la Mbeya lipo.

Je, Mheshimiwa Waziri, uko tayari kukutana na Wabunge wa miji hiyo 45 ili kutueleza maendeleo ya mradi huo kama tulivyofanya kwenye miji 28 maji?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, nitamwambia Waziri wa Nchi na tutakutana na Wabunge wote katika hiyo miji 45 ili kuwaelezea juu ya utekeleza wa mradi huo. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, je, Serikali ina mpango gani wa kuzitumia fedha zilizobaki katika utekelezaji wa mradi huu wa DMDP Awamu ya Kwanza katika kuziboresha barabara za Jimbo la Mbagala na Jimbo la Temeke?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Chaurembo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumepokea ushauri na tutakwenda kushauriana na wataalam juu ya utekelezaji wa mabaki wa hizo fedha ambazo zimebakia, ahsante sana.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanua wigo wa miradi ya kuboresha barabara za mitaa ya Manispaa ya Temeke hasa Jimbo la Temeke kupitia DMDP?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kuniruhusu niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa Jimbo la Kawe, katika Wilaya ya Kinondoni lina mtandao mkubwa wa barabara kuliko majimbo yote ya Dar es Salaam; je, Serikali inaweza kusema ina mkakati gani kuongeza nguvu kuongeza barabara kutengeneza kupitia DMDP awamu ya pili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Jimbo la Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba tunatambua ukubwa wa Jimbo la Kawe kama ilivyo katika majimbo mengine na tunatambua umuhimu wa kuongeza bajeti. Na katika mradi DMDP moja ya vigezo ambavyo umezingatia ni pamoja na ukubwa wa maeneo. Kwa hiyo, mgawanyo utalizingatia ukubwa wa maeneo husika, ahsante sana.