Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 389 2022-06-14

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza ujenzi wa vituo vya afya kote nchini ikiwemo katika Jimbo la Korogwe Vijijini. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imepeleka shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya Mnyuzi na Kerenge katika Jimbo la Korogwe Vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Vituo vya Afya vya Mombo, Bungu na Magoma Serikali inafanya tathmini ya vigezo stahiki kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji.