Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza vituo hivi vitatu vya Bungu, Magoma na Mombo ni vituo vya muda mrefu na vinahudumia eneo kubwa; ni lini sasa hiyo tathmini inafayofanya na Serikali itakamilika ili Serikali ipate nafasi ya kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya maboresho?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, vituo hivi nilivyovitaja karibu kila kituo kimoja kinahudumia tarafa nzima, kata zaidi ya tisa. Zipo kata ambazo tumeziainisha kwa ajili ya vituo vya kimkakati; ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya vituo vya mkakati kwenye Jimbo la Korogwe Vijijini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba vituo hivi vya afya vitatu ni vituo vya siku nyingi na Serikali tayari tulishapeleka wataalamu kufanya tathmini ili kuona majengo yanayohitajika, lakini na gharama ambazo zinazohitajika. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakamilisha mapema iwezekanavyo ili Serikali iweze kutafuta fedha kwa ajili ya kwenda kuongeza majengo yanayopungua katika vituo hivi.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu na vituo vya afya vya kimkakati, Serikali imeshaainisha maeneo yote nchini kote ambayo yanahitaji vituo vya afya vya kimkakati ikiwemo kwenye Jimbo la Korogwe Vijijini na fedha zinatafutwa kwa ajili ya ujenzi kwa hatua kadri ya upatikano wa fedha, ahsante sana.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi kuuliza swali dogo la nyongeza.

Katika Jimbo la Njombe Mjini kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya kupanua Kituo cha Afya cha Njombe Mjini kwa sababu hakina wodi za wanaume. Ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Njombe Mjini ni moja ya vituo ambavyo Serikali tayari imeanza kufanya tathmini ya majengo ambayo yatahitajika ili utanuzi uweze kufanyika na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hiyo itafanyika na tunatafuta fedha kwa ajili ya kupanua Kituo cha Afya cha Njombe.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imejenga kwa mapato yake ya ndani kituo cha afya chenye hadhi ya hospitali eneo la Kalema, Kata ya Ikola, kituo hicho kimekamilika, tatizo lililopo ni ukosefu wa wataalamu na vifaa tiba.

Je, ni lini Serikali itawaunga mkono kwa kuwapelekea vifaa tiba na wataalamu ili kile kituo kianze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana halmashauri hii kwa kujenga kituo cha afya kwa mapato ya ndani, lakini nimwakikishie kwamba katika ajira ambazo zinaendelea hivi sasa ambazo kufikapo Julai Mosi watumishi watapelekwa katika vituo vyetu tutahakikisha kituo hiki pia kinapelekewa watumishi ili kianze kutoa huduma. Lakini katika mwaka ujao wa fedha tumetenga shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba ambavyo vitapelekwa ili kituo hiki kiendelee kutoa huduma za afya, ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 4

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naomba kufahamu ni lini Serikali itatuboreshea Kituo cha Afya cha Isasa kwa maana ya kutujengea wodi ya akina mama pamoja na wodi ya akina baba? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuainisha vituo vyote ambavyo vina majengo pungufu ili kuyajenga kwa awamu. Kwa hiyo, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Juliana Shonza ili tuweze kuona majengo yapi yanapungua, gharama kiasi gani inahitajika ili tuanze kujenga majengo yanayopungua, ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 5

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, Kituo cha Afya Msandamuungano ni kati ya vituo vya afya vilivyoko ndani ya Jimbo la Kwela na kina miundombinu chakavu kimekuwa cha muda mrefu; je, Serikali mna mpango gani wa kuboresha hiki kituo cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumefanya tathmini ya vituo vyote kote nchini, vituo chakavu, hospitali chakavu ambazo zitapangiwa bajeti kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Tumeanza na hospitali za halmashauri, lakini tutakwenda na vituo vya afya ili kuvikarabati au kuviongezea majengo. Kwa hiyo naomba nichukue hoja yako Mheshimiwa Sangu ili tufanye tathmini pia katika kituo hicho na kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati na kuongeza majengo ya maeneo hayo, ahsante sana.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Kata ya Kitanga iko kilometa 77 kutoka yalipo makao makuu ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika kata hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kigezo kimojawapo cha kujenga vituo vya afya ni umbali wa eneo hilo husika kutoka kituo cha afya au hospitali ya karibu. Kwa hiyo kwa kilometa 77 bila shaka tunahitaji kuwa na kituo cha afya. Niagize Mkurugenzi wa Halmashauri hii kuhakikisha wanafanya tathmini ya kutafuta eneo, lakini pia watuletee maombi hayo kwa ajili kujenga kituo cha afya katika eneo hilo, ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaboresha na kupanua Kituo cha Afya cha Mvomero? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye mpango mkakati wa kupanua na kuboresha vituo vya afya tutahakikisha pia tunakifanyia tathmini kituo hicho na kutenga fedha ili tuende kukarabati na kupanua kituoo hicho kwa awamu, ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 8

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa pale mkoani Rukwa kwa sababu tayari eneo limetengwa, lakini Serikali bado haijaanza ujenzi. Ni lini Serikali itaanza ujenzi? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye bajeti ya mwaka huu imepangiwa kwa ajili ya kufanya ujenzi kwenye eneo ambalo amelitaja.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 9

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Napenda kuiuliza Serikali je, ni lini Serikali itaanza kujenga vituo vya afya katika kata za kimkakati za Kibata, Kandawale na Miguruwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka huu wa fedha peke yake Serikali imeendelea kujenga vituo vya afya katika maeneo ya kimkakati na mpaka Juni hii tayari tumeshajenga vituo vya afya 234 nchini kote na mpango huu ni endelevu, tutahakikisha tunaendelea kujenga vituo vya afya ikiwemo katika Jimbo la Kilwa Kaskazini, ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuboresha na kupanua Vituo vya Afya vya Bungu, Magama na Mombo ambavyo vinahudumia wananchi wengi?

Supplementary Question 10

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Kata ya Buswelu walijenga hospitali. Baada ya ukaguzi ikaonekana maeneo yale ni madogo ikahamishiwa Kata ya Sangabuya kwa ahadi kwamba maeneo yale yatakuja kupewa kituo cha afya. Lakini leo ni zaidi ya miaka minne hayajawa kituo cha afya.

Je, ni lini Serikali itaweka kituo cha afya katika majengo yale yaliyoko Kata ya Buswelu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwezi uliopita nilitembelea eneo hili la Kata ya Ilemela eneo la Buswelu na kuona yale majengo ambayo yamejengwa na Wizara ya Afya, lakini na jengo moja ambalo lilijengwa kwa ajili ya kituo cha afya, na nilitoa maelekezo majengo yale ifikapo mwisho wa mwaka ujao wa fedha yaanze kutoa huduma kama kituo cha afya badala ya kubaki bila kutoa huduma. Kwa hiyo, tumeshalifanyia kazi hilo na nimwakikishie kwamba litakwenda kukamilika, ahsante.