Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 390 2022-06-14

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Zahanati ya Maisome kuwa Kituo cha Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa miongozo ukubwa wa eneo la kituo cha afya linatakiwa kuwa na angalau ekari nne katika maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Spika, Serikali haikuipandisha hadhi Zahanati ya Maisome iliyopo Kijiji cha Kanoni kuwa Kituo cha Afya kwa sababu ya kukosa eneo la ujenzi. Aidha, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepeleka shilingi milioni 500 kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya kwenye Kata ya Maisome, Kijiji cha Kanoni. Ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje na jengo la maabara upo katika hatua ya ukamilishaji na ujenzi wa majengo ya wodi ya wazazi, jengo la upasuaji, jengo la kufulia na kichomea taka upo hatua ya awali, ahsante.