Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Zahanati ya Maisome kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri. Zangu ni shukrani kwa sababu Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kituo hiki kijengwe baada ya mama mmoja kufia kwenye mtumbwi. Sasa nina swali moja tu la nyongeza.

Je, Serikali iko tayari kuifikiria Kata ya Bukokwa ambayo ina sifa zile zile kama Kisiwa cha Maisome ili iweze kupata kituo cha afya? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchoswa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee shukrani zake nyingi sana kwa Serikali ya Awamu ya Sita na Mheshimiwa Rais wetu kwa kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo la Buchosa na nchini kote kwa ujumla, na nimwakikishie tu kwamba kata hii ambayo ameisema ameshakuja kufatilia mara nyingi kuhusiana na uhitaji wa kituo cha afya na tayari tumeanza kufanya tathmini kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Zahanati ya Maisome kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na Mufindi kwa ujumla makao yake makuu iko kwenye Kata ya Mtwango, lakini eneo hilo mpaka sasa pamoja na kwamba imehamishiwa makao makuu Mafinga Kata ya Mtwango yenye population kubwa haina kituo cha afya; je, ni lini Serikali sasa itapeleka kituo cha afya pale kwa ajili kuhudumia kata hiyo na kata jirani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kata hii ya Mtwango ni kata kubwa na ina wananchi wengi na Mheshimiwa Mbunge ameisemea mara nyingi na tumekubaliana tunatafuta fedha kwenda kujenga kituo cha afya katika kata hiyo, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Zahanati ya Maisome kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 3

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi; Kijiji cha Kizota Kata ya Muungano, Kindimbachini wanajenga zahanati tangu mwaka 2013, je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi hawa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Benaya Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka uliopita peke yake ambao tunaumaliza Juni 30 Serikali imejenga jumla maboma 574 ya zahanati, lakini mwaka ujao wa fedha Serikali imetanga shilingi bilioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa maboma 300 ya zahanati kuchangia nguvu za wananchi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutakwenda kuona pia uwezekano wa kupeleka fedha kwenye boma hilo la zahanati, ahsante.