Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 391 2022-06-14

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: -

Je, Serikali inadaiwa fedha kiasi gani ilizokopa Mifuko ya Hifadhi za Jamii na kiasi gani cha madeni kimelipwa na kwa utaratibu gani?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikopa fedha kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na deni la michango ya wastaafu waliokuwa katika utumishi kabla ya mwaka 1999. Mchanganuo wa madeni na kiasi kilicholipwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Mfuko wa PSSSF shilingi bilioni 506.88 na imeshalipwa shilingi bilioni 500 kwa utaratibu wa kibajeti; na deni la michango ya wastaafu waliokuwa katika utumishi kabla ya mwaka 1999 shilingi trilioni 4.46 na shilingi trilioni 2.17 zimeshalipwa kwa utaratibu wa hatifungani maalum. Aidha kiasi kilichobaki cha deni la Mfuko wa PSSSF shilingi bilioni 6.88 na shilingi trilioni 2.29 zitalipwa katika bajeti ya mwaka 2022/2023.

(ii) Mfuko wa NSSF shilingi bilioni 292.59 zilizokidhi vigezo baada ya uhakiki wa deni la shilingi bilioni 490.16 zitalipwa katika bajeti ya mwaka 2022/2023; na

(iii) Mfuko wa NHIF shilingi bilioni 80.68 zilizokidhi vigezo baada ya uhakiki wa deni la shilingi bilioni 209.72, zitalipwa katika bajeti ya mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kuhakiki sehemu iliyobaki ya deni la Mfuko wa NSSF na NHIF ili yaweze kujumuishwa katika mpango wa malipo.