Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 394 2022-06-14

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi. Sababu ya hali hiyo ni kwamba, Wilaya ya Chakechake ilikuwa na idadi ndogo ya matukio ya uhalifu na hivyo kituo hicho kilionekana kinatosheleza.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu pamoja na shughuli za kiuchumi ikiwemo biashara, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imepanga kujenga vituo vya polisi katika maeneo ya Vitongoji, Pujini, Wesha na Gombani. Tayari Idara ya Ardhi imetoa eneo la mita za mraba 1,496 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi eneo la Vitongoji. Serikali itaanza kujenga kituo hicho kulingana na mpango wake wa ujenzi hususani katika mwaka wa fedha 2023/2024. Nashukuru.