Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wizara imepata ardhi ya kujenga Kituo kimoja cha Polisi; je, ina mkakati gani wa kupata ardhi kujenga vituo vitatu vilivyobaki?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, eneo la Pujini ni miongoni mwa maeneo yenye uhalifu sana; je, Serikali haioni? Ichukue uharaka wa kujenga kituo hicho cha polisi, ili kulinda mali na usalama wa raia?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, ardhi inahitajika na kupitia Bunge lako tukufu nimtake Kamishna wa Polisi Zanzibar awasiliane na mamlaka ya ardhi katika Wilaya ya Chakechake ili waweze kumpangia ardhi kwa ajili ya kujenga kwenye maeneo hayo niliyoyabaini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu eneo lenye changamoto ya uhalifu, niseme kwamba kwa sasa kwa sababu hakuna fedha za kujenga Kituo cha Polisi, basi Polisi Wilaya ya Chakechake waimarishe doria ili kudhibiti makundi yote ya uhalifu kwenye eneo hilo. Nashukuru.

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 2

MHE. KABULA E. SHITOBELA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kituo cha Polisi Kata ya Kiseke, Ilemela hakina nyumba ya askari na kusababisha kituo kufungwa saa 12.00 jioni. Je, Serikali itakamilisha lini nyumba hiyo ili kuepusha kituo kufungwa saa 12.00 jioni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba eneo la Kiseke ni eneo ambalo lina shughuli nyingi za kiuchumi na kibiashara na msongamano mkubwa wa watu na matukio ya uhalifu yapo, na tunatambua kwa juhudi za Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum na Mbunge wa Jimbo la Ilemela wamekuwa mara kwa mara wakisumbua Wizarani ili waweze kujengewa nyumba hii.

Mheshimiwa Spika, kwa vile wameshaanza ujenzi niahidi tu kwamba kupitia Jeshi la Polisi chini ya Mfuko wa IGP wa Tuzo na Tozo, tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge ili kupata fedha za kukamilisha kituo hicho hasa baada ya kufanya tathmini ya kiwango cha fedha zinazohitajika. Nashukuru.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa Serikali sasa imeamua kujenga vituo hivi vya polisi kuanzia ngazi ya kata. Ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Nyegezi kwa ajili ya Kanda ya Ukanda wa Nyegezi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ni nia ya Serikali kujenga vituo vya polisi, kuimarisha usalama wa raia ngazi ya kata na ni kwa msingi huo tumeweza kutoa askari kata katika kata zote nchini.

Sasa hili suala la ujenzi wa vituo ni suala la gharama na kwamba katika kipindi kifupi hatuwezi kufanya hivyo kulingana na mpango wetu wa ujenzi. Tutaanza na mikoa ambayo haina Ofisi za RPC, lakini Wilaya ambazo hazina vituo vya OCD. Kwa hiyo, vilivyo kwenye ngazi za kata tumuombe Mheshimiwa Mbunge kushirikiana na wadau waanze ujenzi ili Serikali ije isaidie kukamilisha vituo hivyo. Nashukuru.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 4

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kule kwetu Mkoani Mbeya askari wanafanya kazi nzuri sana ya kulinda rai ana mali zao, lakini askari hawa nyumba zao ni chakavu kweli kweli ukizingatia ni Wilaya zote hakuna nyumba za askari ambazo zinaridhisha.

Sasa je, ni lini Serikali itafanya mpango wa kufanya ukarabati kwenye nyumba hizo za askari wetu? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, Mbeya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nitambue kwamba, maeneo mengi ya vituo vya polisi, makazi ya askari katika maeneo hayo ni chakavu sana na ni kwa msingi huo ndio maana tumeanza ukarabati katika maeneo hayo. Na kwa kweli Mbeya kama Mkoa mkubwa ukanda wa Nyanda za Juu Kusini, kipaumbele kimewekwa kule katika mwaka ujao tutatia kipaumbele ukarabati wa nyumba za askari katika Jiji la Mbeya. Nashukuru sana.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, tatizo la usafiri kwa Kituo cha Polisi cha Mavota ambacho kinahusika na ulinzi wa mgodi wa Biharamulo Gold Mine ni kubwa. Tuna kituo pale, lakini hakuna usafiri hata pikipiki.

Sasa ni lini labda Serikali itatusaidia kupata hata usafiri wa pikipiki mbili/tatu ili tuweze kuimarisha ulinzi juu ya wawekezaji ambao wamewekeza katika mgodi ule wa Mavota?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Biharamulo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba vituo vingi vya polisi havina usafiri wa uhakika, hasa vituo vilivvyo kwenye ngazi ya kata na kwenye maeneo mahususi kama haya ya migodi. Pengine nitumie nafasi hii kueleza kwamba katika mwaka wa fedha huu na ujao tuna magari zaidi ya 300 ambayo yatapatikana na sehemu ya magari hayo ni ku-support usafiri kwenye vituo mbalimbali vya polisi. Sasa pengine niwasiliane na Mbunge kuona uhitaji wa usafiri wa pikipiki katika kituo hiki ili tushirikiane kuzungumza na wadau waweze kutoa fedha kuwezesha ikiwa mpango wa Serikali wa magari hayo utachelewa kufika. Nashukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, ninaomba niulize swali la nyongeza kwamba Wilaya ya Sikonge ambayo ni miongoni mwa Wilaya kubwa kieneo la kijiografia haina kituo chenye hadhi ya Kituo Kikuu cha Polisi cha Wilaya, badala yake wanatumia jengo dogo ambalo lilijengwa na chifu mwaka 1957. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Kituo cha Polisi cha Wilaya? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya nyingi za polisi hazina majengo ya polisi ya ngazi ya Wilaya na ndio maana kama mnakumbuka Waheshimiwa Wabunge kwenye bajeti hii tumezungumzia haja ya kuanza kujenga vituo vya polisi ngazi ya Mkoa na Wilaya kule ambako vituo hivyo havipo. Sikonge najua ni eneo ambalo pia halina hadhi hiyo, kwa hiyo, tutaweka kipaumbele Mheshimiwa Mbunge ili katika mwaka ujao iweze kuzingatiwa katika bajeti tayari tuanze ujenzi wa kituo hicho. Nashukuru sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 7

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Kituo cha Polisi cha Kigonga kinahudumia wananchi waliopo mpakani mwa Tanzania na Kenya wa kata za Itirio, Nyanungu, Mlimba na Gorong’a, lakini kituo hiki kilijengwa kwa full-suit ya mabati kana kwamba kimechakaa na polisi wamekimbia hawapo tena pale.

Sasa ningetaka kujua ni lini Serikali itajenga kituo hiki kwa sababu ni kituo cha kimkakati ukizingatia kipo mpakani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, viwango vyetu vya kujenga vituo vya polisi siyo kuwa full-suit ya mabati, kwa hiyo kama kuna kituo cha aina hiyo hakikidhi viwango pengine sasa niwasiliane na Mheshimiwa Mbunge na mamlaka ya Serikali za Mitaa kule Temeke ili tuanze mkakati wa kujenga kituo kwa kutumia vifaa vya kudumu ikiwa ni matofali na kadhalika...

MBUNGE FULANI: Tarime.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Tarime vijijini yes, kwa hiyo nachukua ahadi...

SPIKA: Waheshimiwa hapa mnapenda kuwazungumzisha Mawaziri wakiwa wanazungumza mwache amalize jibu lake, ukiwa unaongea naye anaanza kuongea na wewe badala ya kuongea na mimi hapa mbele.

Mheshimiwa Naibu Waziri malizia majibu yako.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru nilikuwa nasema hatuna vituo vinavyopaswa kuwa vya polisi vyenye kujengwa kwa full-suit za mabati kwa hiyo kituo hiki kama kweli kipo kule mpakani tutashirikiana na uongozi wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime Rorya ili kuwa na mpango wa kujenga kituo hiki kwa aina ya vifaa vinavyostahiki kujengea kituo cha polisi. Kwa hiyo, nimuondoe mashaka Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaweka kipaumbele na kwa vile kituo kiko mpakani, kilete taswira nzuri ya kituo stahiki katika nchi yetu, nashukuru sana.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni kwa nini hadi sasa Wilaya ya Chakechake ina kituo kimoja cha polisi?

Supplementary Question 8

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini hatuna kabisa kituo cha polisi; je, ni lini Serikali itatujengea kituo cha polisi katika halmashauri yetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishaeleza katika maswali niliyojibu muda mfupi uliopita, si wilaya zote zina vituo vya polisi vya ngazi ya wilaya kwa kulitambua hilo ndiyo maana tuna mpango mkakati wa kiwizara wa kujenga vituo vya polisi vya OCD katika kila wilaya kulingana na mpango wetu na kwa mujibu wa upatikanaji wa fedha Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mtwara na kwa umuhimu wa ukanda ule kitapewa kipaumbele, nashukuru sana.