Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 44 Energy and Minerals Wizara ya Madini 395 2022-06-14

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuimarisha usimamizi, upatikanaji na matumizi ya baruti hapa nchini. Ili kurahisisha upatikanaji wa vibali vya baruti Wizara imesogeza huduma hiyo katika Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa yote ya kimadini nchini ikiwemo Chunya. Aidha, Serikali imesajili na kutoa vibali vipya vya biashara ya baruti kwa kampuni 25 ambazo hutoa huduma hiyo hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini katika kipindi cha mpito kwa matumizi ya zebaki imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kushirikiana na Ofisi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kufanya ufuatiliaji wa taratibu za uingizaji na usambazaji wa kemikali ya zebaki nchini ili kubaini changamoto za upatikanaji wa kemikali hiyo na kuandaa takwimu za kiasi cha matumizi ya zebaki ili kujua kiasi kinachohitajika nchini ili kurahisisha utoaji wa vibali vya uingizaji na kuwatambua na kuwasajili waingizaji na wasambazaji wa kemikali ya zebaki nchini kwa mujibu wa Sheria ya Kemikali nchini ili biashara hiyo ifanyike kwa uwazi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kemikali ya zebaki kutumika katika shughuli za ukamatishaji wa dhahabu, tafiti za kisayansi zimebainisha kuwa kemikali hiyo isipotumika vizuri ni hatari kwa afya ya binadamu na mazingira, jambo lililosababisha Serikali kusaini Mkataba wa Minamata (Minamata Convention) ambao utekelezaji wake unapelekea kupunguza matumizi ya zebaki au kuondoa kabisa pale inapowezekana.

Mheshimiwa Spika, kutokana na madhara ya matumizi ya zebaki, Serikali kupitia mradi wa Environmental Health and Pollution Management Program –imeanza kutafuta njia mbadala ya uchenjuaji kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu ili kuondokana na madhara yanayotokana na matumizi ya kemikali hiyo. Mradi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) na kutekelezwa chini ya Baraza la Udhibiti na Usimamizi wa Mazingira (The National Environmental Management Council - NEMC), ahsante.