Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, tunaishukuru Serikali ndani ya muda mfupi imeweza kujenga maghala takribani kumi ndani ya Wilaya ya Chunya kwa ajili ya baruti. Lakini maghala haya yapo pale Chunya mjini na maeneo ya uchimbaji wa dhahabu yako kule vijijini.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba vibali hivi vinaweza kuwafikia wale wafanyabiashara wa baruti kwenye maeneo yale ya uchimbaji kule vijijini?

Swali la pili kwa mujibu wa majibu ya Mheshimiwa Waziri, Serikali imeshaingia Mkataba wa Minamata kwa ajili ya kupunguza matumizi ya zebaki na baadaye kuitokomeza kabisa. Lakini kwa kipindi hiki cha mpito matumizi ya kemikali hii ya zebaki bado inaendelea kutumika kwa ajili ya kuchenjua na ukamatishaji dhahabu.

Je, Serikali ina mpango gani kutoa elimu kwa wachimbaji hawa wadogo wa dhahabu ili madhara yasiendelee kutokea zaidi?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasaka kama ifuatavyo: -

Kwa upande wa swali lake la kwanza napenda kumfahamisha kwamba Serikali imeendelea kuboresha utaratibu wa kuweka urahisi wa upatikanaji na matumizi ya baruti katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kufikia mwaka huu mwezi huu wa sita Waziri wa Madini kwa mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa kifungu cha (8) cha Sheria ya Baruti ya mwaka 1963 Sura ya 45 amepewa mamlaka ya kutoa leseni kwa viwanda vya kutengeneza baruti hapa nchini na tayari kuna viwanda vitatu vimeshapewa hiyo leseni ya kuzalisha baruti jambo ambalo limepelekea kuwepo kwa upatikanaji wa zebaki kwa wingi nchini, lakini sambamba na hilo kifungu Na. 4 cha Sheria ya baruti Sura ya 45 imempa Waziri mamlaka ya kuteua wakaguzi wa baruti na hao sasa wameshateuliwa na wako katika kila Ofisi ya Madini ya Mikoa yetu yote ya madini nchini na wanafanyakazi chini ya Kamishna wa Madini ambaye anawapa kibali cha kutoa leseni za store na masanduku ya kuhifadhia baruti.

Mheshimiwa Spika, kana kwamba hiyo haitoshi, pia anawapa kibali cha kuweza kutoa leseni na mpaka sasa hivi tuna leseni 256 za maghala yaani magazine, leseni 338 za store yaani store yenyewe na leseni 114 za masanduku (storage boxes) ya kuhifadhia baruti na Kamishna kwa kutumia hawa wakaguzi wa baruti amewapa mamlaka ya kushirikiana na ofisi zetu za madini kila mkoa kuhakikisha kwamba baruti zinawafikia wachimbaji wadogo kwa njia iliyo salama na kwa njia rahisi kabisa kupatikana karibu na maeneo ya migodi.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili ambalo anataka kujua kwamba hii zebaki sasa ambayo ni hatarishi kwa mazingira iko katika mikakati ya kwenda kuondolewa matumizi yake, lakini kwa kipindi hiki cha mpito kabla haijaondolewa matumizi yake Serikali inafanya nini kutoa elimu, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mpaka sasa hivi Wizara imeshatoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo zaidi ya 600 na namna salama ya kutumia zebaki.

Katika Mkoa wa Shinyanga tumetoa elimu hiyo katika maeneo ya Mwimbe, Mwambomba, Kalole, Zambazare na Mwakitolyo na katika mwaka huu wa fedha ambayo bajeti yake inakwenda kusomwa leo Bungeni, tunategemea kuendelea kutoa elimu hiyo katika mikoa yote ya kimadini nchini ikiwemo Songea, ikiwemo Chunya, ikiwemo Songwe, Singida, Geita na maeneo mbalimbali ili wachimbaji wadogo waweze kutumia zebaki kwa makini mpaka hapo njia za mbadala zitakapopatikana, ahsante sana.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana matumizi ya zebaki kwenye maeneo yetu wachimbaji wadogo wadogo hasa Jimbo la Msalala yamekuwa na athari kwa wachimbaji wenyewe, lakini pia kwenye mazingira yanayozunguka pale. Sasa kabla Serikali haijaenda kuzuia matumizi ya zebaki ni teknolojia ipi ambayo mmeianzisha kama mbadala wa matumizi ya zebaki?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, nimweleze tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kuna teknolojia mbadala ambayo inaendelea kutumika katika uchenjuaji wa madini ya dhahabu na teknolojia hiyo inaitwa ni cyanide na matumizi ya cyanide ni aina ya utaalam ambao ile kemikali yenyewe inapokuwa imetumika kuchenjua na kukamatwa kwenye mabwawa ya kuchenjulia madini huyeyuka na kupotea hewani bila kuacha madhara yoyote na hiyo ndiyo teknolojia ya kisasa ambayo tunaendelea kutumia na kuendelea kuitambulisha kwa wachimbaji wadogo.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Supplementary Question 3

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Halmashauri ya Mji wa Bunda, Kata ya Guta, Mtaa wa Kinyambwiga kuna uchimbaji wa madini pale lakini kwa sasa kuna mgogoro kati ya wenye mashamba na wenye leseni. Je, ni nini kauli ya Serikali kwenye mgogoro huu?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini na kwa ridhaa yako namuomba Mheshimiwa Mbunge alete swali hilo kama swali la msingi halafu tutalijibu hapa Bungeni. (Makofi)

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na kwa kuwa madini ya Tanzanite yanaruhusiwa kuuzwa duniani kote ikiwa ni pamoja na India na Marekani.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vibali ili madini hayo pia yaweze kuuzwa kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Mwanza na nchi ya Zanzibar?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kumjibu Mheshimiwa Gambo kwamba madini ya Tanzanite ni madini ya kipekee kabisa ambayo yanapatikana nchini Tanzania tu na kwa ajili hiyo Serikali iliweka utaratibu wa kusimamia uzalishaji, uchakataji, uongezaji wake thamani palepale Mererani. Lakini katika kipindi tulichoko sasa hivi tuko katika hatua za kufanya tathmini ya utaratibu uliowekwa na Serikali ambapo baada ya kujiridhisha kwamba kuna utaratibu mwingine mzuri wa kuruhusu madini hayo yauzwe kila mahali ndani ya nchi na nje ya nchi, bila kuathiri uhalisia wa hali iliyokuwepo ya mwanzo ya utoroshaji wa kiholela tutakwenda kuweka utaratibu mahususi ili madini hayo yaweze kuanza kuuzwa popote pale maadam pia yatakuwa yameshaongezewa thamani na kupewa vibali vya kutoka ndani ya eneo la Mererani ambalo ni eneo tengefu kwa sasa.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha utaratibu wa kupata baruti na zebaki unakuwa rahisi na vibali vitolewe kwa ngazi ya kijiji kwa wachimbaji wadogo?

Supplementary Question 5

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujua ni njia gani nzuri Serikali inatumia kwenye matumizi ya cyanide, kwa sababu madhara ya zebaki ni bora zaidi kuliko madhara ya cyanide ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, nipende tu kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba handlings kwa Kiswahili tunasema jinsi unavyo itumia cyanide kwa usahihi kwa kutengeneza yale malambo na kuweka tiling zile za kuzuia ili isivuje chini ya ardhi, ni njia ya uhakika kabisa kwamba ukishaitumia na ukaiacha ika-evaporate ndani ya anga/hewani haiachi madhara yoyote na ni salama zaidi kuliko zink ambayo upoteaji wake au biodegradability yake ni ngumu zaidi ya kuhifadhi katika maeneo ambayo hakutakaa kuwe na leakage.

Kwa hiyo, utaalam wa cyanide siyo mgumu kama ambavyo yeye anadhani na ni wa uhakika zaidi na ni salama zaidi kuliko zebaki.