Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 401 2022-06-17

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa inaenda kuwa Mamlaka kamili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mhesimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura 288 pamoja na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa Mwaka 2014, vigezo na taratibu zinazopaswa kufuatwa ni pamoja na maombi rasmi kuwasilishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI. Ofisi ya Rais TAMISEMI itakapopokea maombi rasmi ya Halmashauri ya Mji Mbarali itafanya uchambuzi na tathmini ya kukidhi vigezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kumekuwa na changamoto za uendeshaji na tija za kuwepo kwa baadhi ya Mamkaka za Miji Midogo. Ofisi ya Rais TAMISEMI inafanya uchambuzi na kubaini tija ya kuendelea kuwepo au la, kwa baadhi ya Mamlaka za Miji Midogo.