Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa inaenda kuwa Mamlaka kamili?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi, iliyoko Wilaya ya Mbeya yenye watu zaidi ya laki moja iliishapita vigezo vyote vya vikao vyote vya DCC, RCC na hata kiuchumi iko vizuri. Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi itapanda kuwa Halmashauri ya Mji?

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, aliagiza hata kubadili Jina la Jimbo la Mbeya Vijijini. Je, ni lini Serikali itabadili jina la Jimbo la Mbeya Vijijini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Njeza Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji Mdogo wa Mbalizi ni kweli kwamba ni mamlaka ya Mji ya muda mrefu lakini tayari imeshafikisha vigezo kwa maana ya idadi ya watu, uwezo wa kiuchumi, lakini wameshafuata taratibu na kuwasilisha ofisi ya Rais TAMISEMI. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais – TAMISEMI sasa tunafanya tathmini lakini pia tunatambua vigezo hivyo na baadaye tutatawakilisha kwa mamlaka husika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa kadri itakavyokuwa inafaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na jina la Halmashauri ya Jimbo la Mbeya Vijijini kubadilishwa ni taratibu ambazo zinafanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa hivyo Ofisi ya Rais – TAMISEMI tumechkua hili tutashirikiana na Wizara husika kuona uwezekano wa kutekeleza maelekezo hayo ya Mheshimiwa Rais.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa inaenda kuwa Mamlaka kamili?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri, amezungumza kwamba moja ya vigezo vya kupata Halmashauri ni maombi ya Halmashauri husika kufika TAMISEMI. Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imeshaomba kwa miaka mitano mfululizo kuanzisha Halmashauri katika Jimbo la Mikumi, tuna vigezo vyote ambavyo vingine vimepitiliza.

Je, ni nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa Jimbo la Mikumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Kilosa ina Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi, na ninafahamu kwamba vikao vya awali vya kuomba kupandishwa hadhi kuwa halmashauri ya Mji vimeanza, kwa ngazi ya DCC, lakini nafahamu kwamba RCC bado haijakaa kupitisha maombi hayo. Kwa hiyo, nimwelekeze Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kufanya mapema suala hili ili tuweze kuona kama inakidhi vigezo hivyo baada ya kuwasilishwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa inaenda kuwa Mamlaka kamili?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Ningependa kujua Halmashauri ya Bunda ina Majimbo mawili ambayo Halmashauri moja ipo Jimbo la Mwibara lakini Majimbo hayakutani, yamekatwa katikati na Jimbo la Bunda Mjini. Ni lini sasa Serikali itapeleka Halmashauri ya Nyamswa kwenye Jimbo la Bunda Vijijijini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniface Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu maombi ya kuanzisha mamlaka mpya kwa maana ya Halmashauri ya Nyamswa, nimuombe Mheshimiwa Mbunge lakini nimuelekeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, kuanza taratibu ambazo ziko kwa mujibu wa Sheria Sura 288 na kuwasilisha Ofisi ya Rais TAMISEMI ili tuweze kufanya tathmini ya vigezo hivyo. Ahsante.