Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 402 2022-06-17

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: -

Je ni lini ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Nassa itatekelezwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Mwongozo wa Uanzishaji na Usajili wa Shule wa Mwaka 2020 uliotolewa na Wizara ya Elimu unabainisha hatua za kuipandisha hadhi shule kuwa ya Kidato cha Tano na Sita kama ifuatavyo: -

Mwombaji ambae ni Mkurugenzi ataandika barua kwa Kamishna wa Elimu kupitia Mdhibiti Mkuu wa Ubora wa Shule Kanda. Barua hiyo itaambatishwa na taarifa ya ukaguzi wa Mdhibiti wa Ubora wa Shule Kanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kutenga fedha kupitia mapato ya ndani ili kukamilisha miundombinu muhimu inayowezesha shule hii kukidhi vigezo vya kupandishwa hadhi ya kuwa na Kidato cha Tano na cha Sita.